Friday, July 24, 2009

Somo la 5:Kutembea Nuruni: Kuyakana Mambo ya Ulimwengu


(1 Yohana 2)

1, 2 & 3 Yohana: Somo la 5

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sememu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kizulu, nk.

Utangulizi: Kuishi pembezoni mwa bahari inamaanisha kuwa natumia muda mwingi ufukweni kuliko nilivyokuwa nafanya huko nyuma. Mara kwa mara nawaona wanawake wa kiislam wakiwa ufukweni. Tofauti kati yao na watu wengine wa kawaida wanaotembelea ufukweni ni dhahiri. Inanikumbusha nilipokuwa kijana na washiriki wa kanisani kwangu walikuja siku ya Sabato karibu na fukwe za karibu za Ziwa Michigan. Mara kwa mara washiriki wa kanisa bado walikuwa wakivaa suti na mavazi ya kikanisa, wakati ambapo watu waliokuwa wakiota jua walikuwa vakivaa vitu tofauti kabisa. Somo letu la juma hili ni kuhusu "mambo ya ulimwengu." Je, mifano hii miwili ni ya kuyakana "mambo ya ulimwengu"? Is sticking out like a sore thumb God's goal for us? Au, hiyo ni kuifanya kauli ya wazi kwa ulimwengu? Hebu tujivinjari kwenye somo letu la Biblia na kuona kile ambacho Yohana anatufundisha kuhusu mambo ya ulimwengu!

  1. Watoto, Wanaume na Akina Baba
    1. Soma 1 Yohana 2:12-13. Yohana anasema anawaandikia watoto, akina baba na vijana. Je, hiyo ndiyo sababu tuna nyaraka tatu: Yohana wa kwanza, pili na tatu?
      1. Kama ndio hivyo, kwa nini Yohana anaonyesha makundi mengine mawili katika Yohana wa Kwanza? (Yohana hana waraka mwingine kwa kila kundi.)
      2. Je, Yohana ana ujumbe wa aina tatu tofauti kutegemeana na kundi linaloelezewa?
      3. Kwa nini wanawake wameachwa, yaani, hawakutajwa kwenye ujumbe? Je, wao tayari ni wenye haki?
    2. Hebu kwanza tuwaangalie watoto. Fungu linasema kwamba wamesamehewa dhambi zao na kwamba wamemjua baba. Je, hilo siyo kweli pia kwa makundi yote matatu? (Nafikiri Yohana anazungumzia waumini wapya, siyo watoto kikwelikweli. Muumini mpya anaweza asiwe na uelewa mpana wa injili. Hata hivyo muumini mpya ambaye alikuwa Myahudi aliyebadili dini ange "mjua Baba," ikimaanisha Mungu wa Agano la Kale. Muumini mpya angekuwa katika jukwaa la uelewa kwamba Yesu alikuwa kafara "mpya" ya dhambi. Sababu ambayo Yohana hawataji wanawake ni kwamba anaandika kuhusu kukomaa kiroho, siyo jinsia.)
    3. Tuna ujumbe gani kwa akina baba-Wakristo waliokomaa? ("Umemjua Yeye ambaye yupo tangu mwanzo.")
      1. Unadhani hili linamaanisha nini? (Kama tulivyoona hapo awali, hili linamrejea Yesu (Yohana 1 na 1 Yohana 1). Hawa ni Wakristo walio na uelewa wa Yesu.)
    4. Tuna ujumbe gani kwa "vijana?" (Wamemshinda mwovu.)
      1. Tunawezaje kusema kwamba mwanadamu yeyote "anamshinda mwovu?" (Hawa ni Wakristo wanaokua. Wanatambua kwamba Yesu amewasamehe dhambi, lakini wana mwendo wa kiroho kuelekea kwenye haki. Wanaweka lengo la kila siku la utii.)
    5. Soma 1 Yohana 2:14. Ni kitu gani kingine tunachojifunza kuhusu "vijana?" (Neno la Mungu hukaa ndani yao. Wanasoma neno la Mungu. Wanamtegemea Roho Mtakatifu.)
    6. Hebu tufanye tathmini: Yohana anawaandikia waumini wa madaraja yote ya ukomavu wa Kikristo. Anasifia  kila kundi katika maendeleo waliyoyafikia hadi sasa. Kinachofuata, tunageukia ujumbe wake kwa makundi yote.
  2. Kuipenda Dunia
    1. Soma 1 Yohana 2:15. Kila kitu ninachokijua na kukigusa na nilichokizoea kipo "duniani". Nawezaje nisikipende?
      1. Kwa kuwa tumeambiwa kuwa kuipenda dunia ni kinyume na kumpenda Mungu, unadhani inamaanisha nini kusema kuwa "dunia" na "chochote kilichomo duniani?"
    2. Soma 1 Yohana 2:16. Tunaona nini "duniani?" (uchu, tamaa ya mwili na kujisifu/kujigamba.)
      1. Je, "mambo" haya yamo "duniani?" (Hapana. Hii ni mitazamo kuhusu vitu fulani.)
      2. Hebu tuangalie hili kidogo. Kama Yohana anaongelea kuhusu mambo ya ulimwengu, je, anatufundisha kwamba mambo ya ulimwengu ni mtazamo au matarajio?
        1. Kama habari ndiyo hiyo, kuna uhusiano gani kati ya jinsi Mkristo anavyovyaa na mtizamo wa Mkristo?
          1. Hili linasema nini kuhusu "vazi la ufukweni" nililolielezea kwenye utangulizi? Je, kujivika, au kuvaa mavazi tofauti, ni kukataa/kukana mambo ya ulimwengu?
      3. Kama uchu, tamaa ya mwili na kujisifu/kujigamba ni mitizamo kuhusu vitu fulani, je, hiyo inamaanisha kuwa watu wasio na vitu (masikini) wanaweza kuwa wa dunia? (Kinyume chake ni kwamba wale wasio na vitu wanaweza kuwa na matatizo mengi kuhusiana na hili kuliko wale walio na vitu na kuamua kuwa "vitu" siyo vya msingi kihivyo.)
    3. Soma tena 1 Yohana 2:16. Kauli "cravings of sinful man," inatafsiriwa kuwa "tamaa ya mwili."  Hii inatusaidiaje kujua kile inachomaanisha? (Mtu aliye na tamaa hizi (hii "tamaa") ana mtazamo juu ya mambo ya kidunia.)
      1. Vipi kuhusu wewe? Una mtazamo wa kidunia? Unatamani vitu fulani? Unatamani ungekuwa na vitu fulani?
    4. Tulipokuwa tukielekea kanisani wiki iliyopita, mimi na mke wangu tulikuwa tukiongelea mambo ya mbeleni. Tunapanga kuuza nyumba yetu ya sasa na tulikuwa tunajadili kuhusu mahala pengine pazuri/bora pa kuishi. Mahala pazuri kwangu ni nyumba hii (hapa tunapotaka kupauza) karibu kabisa na ufukwe ambapo unaangalia ghuba ya Chesapeake na bahari ya Atlantiki. Gharama? Dola milioni 1.3. mke wangu angependa kuishi katika milima ya  Blue Ridge-takriban saa 3 kutoka ufukweni. Nikasema, "Kama tungekuwa na pesa za ziada kidogo tungejipanga"-ikimaanisha kwamba tungeweza kununua nyumba ya ufukweni na nyumba iliyopo katika milima ya Blue Ridge . Je, hizo ni "tamaa za mdhambi" na "tamaa za macho yake?" (Ndiyo! Angalao kama inaelekea kwenye hatua ya uchu na kutamani tofauti na kuchukulia kwamba mambo haya hayawezekani.)
    5. 1 Yohana 2:16 inamaanisha nini inaporejea "tamaa ya macho yake?" (Unataka kile unachokiona.)
      1. Kwa nini hili ni makosa? (Vitu vya kiroho kwa ujumla huwa havionekani. Vitu vya kiroho mara kwa mara huwa ni mahusiano. Kwa hiyo, unatamani juu ya mambo mabaya/yasiyostahili katika maisha.)
    6. 1 John 2:16 inarejea kitu gani inapoongelea "kusaidia kile alichonacho na akifanyacho?" (Huu ni mshale moyoni mwangu. Mara zote nimekuwa nikifurahia kuwa mwanasheria. Napenda kusema kuwa mimi ni mwalimu wa shule ya sheria kwa sababu inapendekeza kuwa mimi siyo mwanasheria tu, bali mwanasheria mwerevu. Hili ndilo linaonekana kwa hakika Yohana analishutumu kuwa la kidunia. Kama mtu yeyote anataka kuniokoa kwa kupendekeza tafsiri nyingine, nipo wazi kulisikiloiza! Kwa sasa ninatubu.)
  3. Mtazamo wa mbali
    1. Soma 1 Yohana 2:17. Kuna shida gani na aina hizo za matamanio? Haya mambo ya ulimwengu?
      1. Je, Yohana anasema kwamba mtazamo wa kidunia, kuwa na hisia kuhusu kuwa na "vitu" ni dhambi? Au tu ni kujishughulisha/kujifikirisha kipumbavu?
      2. Kama mtu hampendi Mungu, je, hiyo siyo ishara ya "dhambi?" (Yote haya yana mantiki kwangu. Kama tunajishughulisha na kupata vitu, basi hatujishughulishi na kumjua Mungu. Mathayo 6:24 inasema kwamba fedha ni bwana. Hatuwezi panda na kumtumikia Mungu na pesa. We cannot love and serve both God and money.)
      3. Umewahi kusikia msemo "ilikuwa nzuri wakati ambapo ilikaa kwa muda mrefu?" Je, linahusika hapa-kwenye kauli ya 1 Yohana 2:17? 
      4. Mungu anatupatia kitu gani kilicho bora sana? (Uzima wa milele! Vitu vya milele. Nadhani Yohana anajenga hoja kivitendo. Kile ulicho nacho na vile jinsi ulivyo sasa ni vya muda tu. Pale unapokufa, nani anakumbuka au anajali? Pesa yako inakwenda kwa mtu mwingine. Inaleta mantiki gani kujishughulisha na kitu ambacho kwa hakika utakipoteza? Kwa upande mwingine, Mungu anatupatia vitu vya milele na sifa njema.)
    2. Una ufahamu wa kiasi gani kuhusu babu zako wa mbali sana (mababu wa babu zako)? (Nilipokuwa ninaandika somo hili, mke wangu alipata na kunitumia kipande cha picha ya video kuhusu kujiuzulu kwa baba yangu katika wadhifa wake wa mwisho. Kitini hicho kilikuwa na kichwa cha habari kikubwa na picha ikionyesha kwamba baba yangu alikuwa mtu mzuri sana wa sura. Lakini kitini hicho ni kama vile hakikuelezea chochote kuhusu kazi yake au mafanikio yake. Badala yake, kilitaarifu kuwa alikuwa na ugonjwa wa moyo, kikaonyesha kiasi alichopata (pesa) na kwamba walikuwa watafuta mtu mbadala. Kile tulichonacho na kile tunachokifanya, yote ni ya muda tu!)
    3. Rafiki, vipi kukuhusu wewe? Unatizamia umilele au mambo ya dunia hii? Kwa nini usiamue leo kutizamia kwenye mambo ambayo hayataisha kamwe! Habari gani kuhusu kuwa wa "kimbingu" badala yaw a "kidunia?"
  4. Wiki Ijayo: Kutembea Nuruni: Kuwakataa Wapinga Kristo.


 

Kama ilivyofasiriwa na Mgune Masatu.

No comments:

Post a Comment