Tuesday, October 6, 2009

SOMO LA PILI: KUWAANDAA WATU

Hesabu 5 & 6: Somo la 2

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kizulu, nk.

Utangulizi: Wasomaji wasio na uzoefu wa Agano la Kale wanaweza kuudhika/kughafilika pale wanaposoma sura mbili za kitabu cha Hesabu ambacho tunazisoma hivi leo. Kwa kuwa sisi siyo walengwa, wala hatupo katika mazingira yao (kundi kubwa likisafiri kwenye jangwa la kutisha), siyo sehemu ya mfumo wa hekalu, waweza kuuliza “Kuna haja gani kwanza tujifunze haya?” Wakristo wengi wanaamini kwamba kile kilichoandikwa kwenye Biblia kina ushauri usio na kikomo wa vizazi vyote vya wafuasi wa Mungu. Kuna kanuni (na huenda zaidi) katika kitabu cha Hesabu zinazoendelea kutufundisha kuhusu njia za Mungu na mipango yake na matarajio yake kwetu. Hebu tuzame kwenye somo hili la kuvutia!

I. Matengenezo ya Kiafya

A. Soma Hesabu 5:1-3. Je, hivi ndivyo ambavyo ungemtendea mgonjwa?
1. Je, watu wote walioelezewa hapa ni wagonjwa? (Hapana. Wengine ni “najisi kimapokeo ama kutokana na taratibu tu.")
2. Kama si kila mmoja aliyetolewa ni mgonjwa, je, hili linaleta mantiki gani kwetu hivi leo? (Mtu aliyefariki aweza asiwe amekufa kutokana na uzee. Kwa vile mtu aliye “najisi” amegusa maiti, wanaweza pia kuwa wametwaa baadhi ya magonjwa hatari ya kuambukiza.)
3. Unapotafakari hizi kanuni, je, ni kwa ajili ya manufaa ya watu au la? Je, zina huruma au la? (Pamoja na hawa watu wote wanaosafiri katika hali ya mawasiliano ya ukaribu, kuwatenga wagonjwa (na wale wanaoweza kuambukiza wengine) hadi pale wanapopona, au wanapothibitishwa kuwa hawana magonjwa tena, ni mbaraka mkubwa kwa wote waliosalia.)
B. Angalia tena Hesabu 5:3. Kwa nini Mungu anapendekeza kuwa kanuni hii inahusika naye na si afya za watu? (Mungu ndiye mmiliki wa watu hawa. Ni wake yeye. Anataka kambi lenye afya kwa ajili ya watu wake. Inatukumbusha juu ya asili takatifu ya Mungu.)
1. Tunajifunza somo gani hapa tunapofikiri kwamba Mungu “anadhibiti uhuru wetu” na kanuni zake za kiholela au zisizo na msingi? (Mungu kwa uhakika anatutafuta. Tunaweza kufikiri kwamba kanuni zake ni za kiholela, lakini anatujali na kututhamini mawazoni mwake.)
C. Soma Hesabu 5:4. Unafikiri hawa watumwa walioachiwa hivi punde wanaelewa kwa nini Mungu aliweka hivi vigezo? (Inawezekana hawakuelewa sababu, lakini habari njema ni kwamba walitii.)

II. Mageuzi ya Kisheria
A. Soma Hesabu 5:5-7. Nini lalamiko lako kubwa kuhusu mfumo wa sheria za makosa ya jinai? (Nchini Marekani, lalamiko moja kubwa ni kwamba kama anazo, basi mwathirika ana haki chache. Mara chache sana mwathirika anafidiwa kwa madhara aliyoyapata.)
1. Biblia inapendekeza adhabu gani? (Kwamba mwathirika si tu ana haki ya kufidiwa kikamilifu, lakini pia malipo ya ziada ya 20% kwa athari alizozipata.)
2. Nchini Marekani, kwa ujumla mwenye hatia anafungwa gerezani. Mfumo upi ni bora? Mfumo wa Biblia au mfumo wa Marekani? Idadi (nayo ni kubwa) ya wafungwa inahusisha wakosaji wasio na vurugu. Walipa kodi hugharimika – kuwalisha, kuwalaza na kuwavisha watu waliomo magerezani. Mfumo wa Marekani huhitaji fedha nyingi-fedha zinazotoka kwa watu wasio na hatia na ambazo hazielekezwi kuwasaidia waathirika wasio na hatia. Vilevile, haionekani kuwasaidi sana wenye hatia isipokuwa kuwafungilia mbali nasi)
B. Ona jinsi Hesabu 5:6 inasema kuwa mtenda dhambi “siyo mwaminifu kwa Bwana.” Hili lina ukweli gani? Je, mtenda dhambi siyo mwaminifu kwa mhanga? (Hawa sasa ndiyo waliokuwa watu wa Mungu pamoja naye safarini. Aliwaumba yeye, hivyo kushindwa kokote kuishi kutokana na viwango vyake ni kumkosea yeye)
1. Je, kuna dhana yoyote hafifu kama hii hivi leo? (Nina uzoefu na mfumo wa jinai wa Marekani tu, nao ni kama huu kabisa. Yaani ukivunja sheria, lalamiko la jinai huletwa katika jina la Jamhuri. Mamlaka kuu inasema, “Hizi sheria ni zangu ili kuwalinda watu, nanyi mmetenda kinyume dhidi yangu. Hivyo umenikosea mimi.” (yaani jamhuri inamtangazia mhalifu kwamba mhalifu ameikosea jamhuri kwa kuhalifu sheria zake za kuwalinda watu wake yeye Jamhuri).
2. Hesabu 5:7 inasema kuwa mtu lazima aungame. Ungamo linafanywa kwa nani? (Fungu linasema kuwa “dhambi” inaungamwa-na hiyo ni kwa Mungu. Kuna vitu viwili vinaendelea hapa: Kwanza, adhabu ya 20% husawazisha mambo na mtu aliyetendewa kosa. Pili, ungamo husawazisha mambo na Mungu.)

III. Matengenezo ya Ndoa

A. Pitia kwa haraka haraka Hesabu 5:11-28 na usome Hesabu 5:29-30. Una dukuduku gani na huu mwenendo/utaratibu? (Ni kwa nini kwamba mwanamke, na siyo mwanaume, ndiye anapaswa kupitia haya yote? Kwa nini wivu tu ndiyo ujenge huu utaratibu? Wivu waweza kuwa dhambi-na ndiyo ulikuwa msingi kwa mauaji ya kwanza kabisa, sawa? (Mwanzo 4))
1. Je, hii ni adhabu ya kawaida ya uzinzi? (Soma Mambo ya Walawi 20:10. Hii siyo adhabu ya kawaida. Adhabu ya kawaida ni kwamba mwanamke na mwanaume wote waliofanya uzinzi watauawa.
2. Soma Kumbukumbu la Torati 17:6. Ni nini kilichokuwa kinakosekana kwenye “utaratibu wa wivu” wa Hesabu 5? (Hakuna mashahidi. Walihitajika mashahidi wawili au watatu ili kutekeleza adhabu ya kifo katika Mambo ya Walawi 20:10.) concerns
3. Fikiria kwa muda mfupi tu na uweke pembeni mtazamo wako wa kileo/kisasa kuhusu usawa.(wa jinsia) Ni tatizo la aina gani katika aina ya familia iliyoelezewa hapa? (Mashitaka kati ya mume na mke. Ndoa inavunjika. Mahusiano yanaharibiwa yakiwa yamejengwa kwenye mashaka yanayoweza kuwa ya kweli au si ya kweli.)
a. Mpango wa Mungu unatimiza nini? Lengo gani linatoshelezwa na huu utaratibu? (Inaleta mwisho wa wivu na mashaka. Ama Mungu anamdhihirisha mke kuwa hana hatia (ni nani awezaye kubishana na Mungu?), au mke anafariki. Wachambuzi wa Kiyahudi wanasema kwamba mwanamke angeweza kukataa kula kiapo, angeungama, na kutalikiwa tu. Hakuna kifo kwa sababu hakuna ushahidi wa kutosha.)
B. Kuna somo gani kwa ajili yetu leo hii? (Vingi ya tuvionavyo kwenye luninga na kwenye sinema hutukuza uzinzi. Uzinzi ni tatizo la kutisha katika jamii na hata kanisani. Ujumbe/Hoja ya Mungu katika hili ni wa namna mbili: Anachukia uzinzi na anataka kuleta amani kwenye ndoa ambazo tuhuma kama hizi zimeibuliwa. Mungu anataka tatizo hilo liishe, hataki kijinga cha moto kwenye ndoa.)

IV. Mabadiliko ya Kiroho

A. Soma Hesabu 6:1-4. Kumbuka ya kwamba Mungu amewaweka Walawi wakfu. Ni fursa ipi hii inawapatia wale ambao hawakuzaliwa Walawi au wanaume? Je wale ambao hawakuzaliwa wakiwa walawi na wala si wanaume wanapata fursa gani hapa? (Hii inaonyesha kwamba hata katika kipindi cha Agano la Kale, Mungu alitamani kuwa na mahusiano maalum na mtu yeyote aliyekuwa tayari-bila kujali familia au jinsia.)
1. Unafikiri hii inahusianishwa na kanuni iliyotangulia? (Majaribu ya kingono yana nguvu sana . Mtu aliyetizama utaratibu uliotangulia angeweza kuamua kwamba anahitaji muda maalum na Mungu.)
2. Mungu anaelekeza kwamba mtu yeyote anayetaka kuwa na mahusiano maalum naye asiwe anakunywa pombe. Hiyo inahusianaje? (Ni mara ngapi dhambi ya uzinzi inahusisha pombe/ulevi?)
a. Panaonekana kuwepo na sababu dhahiri kwamba kwa nini kuwa mlevi ni kinyume na “nadhiri ya kujiweka wakfu kwa Bwana.” Lakini hii kanuni inakataza maji ya zabibu na hata zabibu kavu-kitu chochote kinachotokana na zabibu. Ni kwa jinsi gani ulaji wa zabibu kavu unaingilia mahusiano na Mungu?
3. Soma Mathayo 26:27-29. Yesu anasema nini kuhusu maisha yake ya baadaye na zabibu? (Kwamba hatakunywa tena hadi tutakapokutana naye mbinguni.)
4. Swali la vitendo: Ulaji wa zabibu na unywaji wa divai ulikuwa na nini hasa kwa watu waliokuwa janwani wakila mana pekee? Je, wote hawakuwa Wanazarayo (kwa kiwango flani) katika kipindi cha safari ya jangwani?
5. Unapokula kwenye sehemu ya kula vyakula vya Kimarekani (Taco Belt), Subway, McDonald au Burger King, je, unakunywa maji? (Si unakunywa soda? Kwa kawaida hizi sehemu zinauza vyakula vikavu pamoja na soda – Fadhili Ndimangwa kama hapo Bangalore huwa anaenda KFC Brigade Road kula kuku ni shahidi wa hili)
a. Vinywaji vyote vya aina ya soda katika sehemu hizi aidha vina caffeine au sukari au vyote. Sipendi kuwa na wasiwasi au kuwa mnene. Kuwa na wasiwasi na mnene ni kubaya sana ! Lakini,maji kwa ujumla yana ladha isiyo na mvuto. Hata kama yangekuwa yana ladha ya kuvutia, wengi wangependelea ladha ya kinywaji cha soda (soda kwa kawaida ina kaboni.))
6. Natumaini nimekufanya utafakari kwamba kwa nini divai ya zabibu inaonekana kuwa na tabia isiyo ya kawaida katika Biblia (na ninaamini hufikirii kuhusu vyakula vya fast food/madukani (vyakula kama vile chips, kuku wa kukaanga, pizza, burger, n.k. ambavyo ukifika tu unachukua na kuondoka au kula papohapo; ndio maana fast food nyingi zinaliwa pamoja na soda na sio mchuzi au supu, they are fast food, vya kula haraka haraka ukiwa safarini ama kwa hamu tu na sio kwenda kula kushiba ukiwa na njaa kali ama kula chakula bora). Kuna nini kuhusu divai ya zabibu (na mazao ya zabibu) ambacho ni maalum sana-ukilinganishwa na mahusiano maalum na Mungu? (Mara zote nimekuwa nikitafakari kuwa inahusisha kujikana nafsi. Jikane nafsi na utakuwa na mahusiano ya karibu na Mungu. Lakini, Frank Holbrook amenisaidia kutizama kwa undani zaidi. Alisema kwamba kupanda mizabibu ilionyesha kuwa umeweka makazi yako katika ardhi/nchi. Yesu “hajaweka makazi” hadi pale tutakapounganishwa naye tena. Hatupaswi kupiga kambi kwa mahusiano ya dhaifu na Mungu. Tunapaswa kuwa njiani kuelekea kwenye mahusiano bora na nyumbani kwetu pa milele!

V. Mibaraka ya Mwisho
A. Soma Hesabu 6:22-27. Rafiki, ungependa huu mbaraka? Unatoka kwa Mungu yule yule anayetupa maelekezo ya jinsi ya kuishi. Hebu fikiria hilo ? Mahusiano kati ya jinsi tunavyoishi na mibaraka ya Mungu!

VI. Juma lijalo: Ibada na Kujitoa wakfu

Wednesday, September 2, 2009

LETTERS TO YOUNG LOVERS - 2

From the Writings of Ellen White

I write because I love your soul.-- Letter 51, 1889.
Dear youth, I wish to speak decidedly to you, because I want you to be saved.-- Messages to Young People, p. 140. My dear sister, I have written to you because I have a love for your soul.-- Letter 51, 1894. I do not consider your case hopeless; if I did my pen would not be tracing these lines.-- Testimonies, vol. 2, p. 562.

Take reproof as from God, take counsel and advice given in love.-- Letter 30, 1875. Keep your wants, your joys, your sorrows, your cares, and your fears before God. You cannot burden Him; you cannot weary Him. He who numbers the hairs of your head is not indifferent to the wants of His children.

"The Lord is very pitiful, and of tender mercy." James 5:11. His heart of love is touched by our sorrows and even by our utterances of them. Take to Him everything that perplexes the mind. Nothing is too great for Him to bear, for He holds up worlds, He rules over all the affairs of the universe.

Nothing that in any way concerns our peace is too small for Him to notice. There is no chapter in our experience too dark for Him to read; there is no perplexity too difficult for Him to unravel. No calamity can befall the least of His children, no anxiety harass the soul, no joy cheer, no sincere prayer escape the lips, of which our heavenly Father is unobservant, or in which He takes no immediate interest.

"He healeth the broken in heart, and bindeth up their wounds." Psalm 147:3. The relations between God and each soul are as distinct and full as though there were not another soul upon the earth to share His watchcare, nor another soul for whom He gave His beloved Son.-- Steps to Christ, p. 100.


NEXT WEEK: MARRIAGE A FORETASTE OF HEAVEN

Sunday, August 23, 2009

LETTERS TO YOUNG LOVERS

Letters to Young Lovers
Ellen G. White

Table of Contents
Introduction
1- Marriage--a Foretaste of Heaven
2- Finding the Right Mate
3- Is It Really Love?
4- Looking for Help?
5- In Control
6- Sexual Responsibility
7- Shadow Over the Nest

Introduction

"I LOVE YOU!" HOW SPECIAL ARE THOSE WORDS BETWEEN TWO YOUNG PEOPLE! BUT EVEN MORE WONDERFUL THEY BECOME WHEN SPOKEN TO US BY OUR SAVIOUR WHO WANTS US TO BE HAPPY AND FIND JOY IN OUR RELATIONSHIP WITH EACH OTHER.

CHRIST HAS COMPARED HIS LOVE FOR THE CHURCH TO THE LOVE OF HUSBAND AND WIFE. THE SCRIPTURES CONTAIN TENDER LOVE STORIES SUCH AS THAT OF JACOB AND RACHEL, AND THE MOVING STORY OF RUTH, THE MOABITE, WHO THROUGH HER MARRIAGE TO BOAZ BECAME A LINK IN THE GENEALOGY OF THE MESSIAH.

OUR HEAVENLY FATHER IS CONCERNED OVER OUR LOVE-LIFE. THROUGH THE INSPIRED WRITINGS OF SCRIPTURE AND OF Ellen White, GOD HAS GIVEN COUNSELS TO YOUNG PEOPLE IN THEIR QUEST FOR HAPPINESS.

FROM THE BIBLE

"BEHOLD, WHAT MANNER OF LOVE THE FATHER HATH BESTOWED UPON US, THAT WE SHOULD BE CALLED THE SONS OF GOD" (1 JOHN 3:1). "I AM COME THAT THEY MIGHT HAVE LIFE, AND MIGHT HAVE IT MORE ABUNDANTLY" (JOHN 10:10). "THESE THINGS HAVE I SPOKEN UNTO YOU, THAT MY JOY MIGHT REMAIN IN YOU, AND THAT YOUR JOY MIGHT BE FULL" (JOHN 15:11).

"HE THAT TOUCHETH YOU TOUCHETH THE APPLE OF HIS EYE"
(ZECHARIAH 2:8). "THIS LOVE OF WHICH I SPEAK IS SLOW TO LOSE PATIENCE--IT LOOKS FOR A WAY OF BEING CONSTRUCTIVE. IT IS NOT POSSESSIVE: IT IS NEITHER ANXIOUS TO IMPRESS NOR DOES IT CHERISH INFLATED IDEAS OF ITS OWN IMPORTANCE.

"LOVE HAS GOOD MANNERS AND DOES NOT PURSUE SELFISH ADVANTAGE. IT IS NOT TOUCHY. IT DOES NOT KEEP ACCOUNT OF EVIL OR GLOAT OVER THE WICKEDNESS OF OTHER PEOPLE. ON THE CONTRARY, IT IS GLAD WITH ALL GOOD MEN WHEN TRUTH PREVAILS. "LOVE KNOWS NO LIMIT TO ITS ENDURANCE, NO END TO ITS TRUST, NO FADING OF ITS HOPE; IT CAN OUTLAST ANYTHING. IT IS, IN FACT, THE ONE THING THAT STILL STANDS WHEN ALL ELSE HAS FALLEN" (1 CORINTHIANS 13: 4-8 PHILLIPS).

"THE LORD HATH APPEARED OF OLD UNTO ME, SAYING, YEA, I HAVE LOVED THEE WITH AN EVERLASTING LOVE; THEREFORE WITH LOVING- KINDNESS HAVE I DRAWN THEE" (JEREMIAH 31:3). "FOR I AM PERSUADED, THAT NEITHER DEATH, NOR LIFE, NOR ANGELS, NOR PRINCIPALITIES, NOR POWERS, NOR THINGS PRESENT, NOR THINGS TO COME, "NOR HEIGHT, NOR DEPTH, NOR ANY OTHER CREATURE, SHALL BE ABLE TO SEPARATE US FROM THE LOVE OF GOD, WHICH IS IN CHRIST JESUS OUR LORD" (ROMANS 8:38, 39).

"HE THAT TOUCHETH YOU TOUCHETH THE APPLE OF HIS EYE"
(ZECHARIAH 2:8). "THIS LOVE OF WHICH I SPEAK IS SLOW TO LOSE PATIENCE--IT LOOKS FOR A WAY OF BEING CONSTRUCTIVE. IT IS NOT POSSESSIVE: IT IS NEITHER ANXIOUS TO IMPRESS NOR DOES IT CHERISH INFLATED IDEAS OF ITS OWN IMPORTANCE.

"LOVE HAS GOOD MANNERS AND DOES NOT PURSUE SELFISH ADVANTAGE. IT IS NOT TOUCHY. IT DOES NOT KEEP ACCOUNT OF EVIL OR GLOAT OVER THE WICKEDNESS OF OTHER PEOPLE. ON THE CONTRARY, IT IS GLAD WITH ALL GOOD MEN WHEN TRUTH PREVAILS.

"LOVE KNOWS NO LIMIT TO ITS ENDURANCE, NO END TO ITS TRUST, NO FADING OF ITS HOPE; IT CAN OUTLAST ANYTHING. IT IS, IN FACT, THE ONE THING THAT STILL STANDS WHEN ALL ELSE HAS FALLEN" (1 CORINTHIANS 13: 4-8 PHILLIPS). "THE LORD HATH APPEARED OF OLD UNTO ME, SAYING, YEA, I HAVE LOVED THEE WITH AN EVERLASTING LOVE; THEREFORE WITH LOVING- KINDNESS HAVE I DRAWN THEE" (JEREMIAH 31:3).

"FOR I AM PERSUADED, THAT NEITHER DEATH, NOR LIFE, NOR ANGELS, NOR PRINCIPALITIES, NOR POWERS, NOR THINGS PRESENT, NOR THINGS TO COME, "NOR HEIGHT, NOR DEPTH, NOR ANY OTHER CREATURE, SHALL BE ABLE TO SEPARATE US FROM THE LOVE OF GOD, WHICH IS IN CHRIST JESUS OUR LORD" (ROMANS 8:38, 39).

Monday, August 17, 2009

SOMO LA NANE : KUWAPENDA NDUGU NA DADA

Kuwapenda Ndugu na Dada

(1 John 3:11-24)

1, 2 & 3 Yohana: Somo la 8

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kizulu, nk. Mwombe Roho Mtakatifu aongoze mawazo yako.

Utangulizi: Juma hili sote tutafakari kama wanasheria wa “common law”. Walianzisha wazo kwamba sheria haikutokana na vifungu bali vifungu vilitokana na maamuzi ya mashauri yaliyopita. Hapa tunamaanisha vifungu vya sheria, yaani legislations. Katika muktadha ya awali, unatumia kifungu Sahihi cha sheria endapo tu uliuliza swala/swali Sahihi, wakati katika muktadha ya pili unaoanisha maamuzi ya mashitaka/mashauri yaliyopita na mashitaka yaliyopo ili kupata jibu/kanuni/kifungu Sahihi). Yohana anatupatia “mambo” fulani ili kuweza kutafakari namna ya kuishi tunapokuwa tukiendelea na safari yetu kwenye njia ya kuelekea kwenye mwanga. Hebu tuzame ndani ya somo letu la Biblia na tuone kile tunachoweza kujifunza kuhuhu kuishi Kibiblia!

I. Kaini Dhidi ya Yesu

A. Juma lililopita tuliishia kwenye somo letu kwa muhtasari wa Yohana wa jinsi tunavyoweza kuwatofautisha watu wema kutoka kwa watu wabaya. Watu wema hufanya vitu vizuri na watu wabaya hufanya mambo mabaya. Hilo lilituacha na swali, “Ni nini, kwa hakika, ni kitu kizuri?” Hebu tuendeleze mjadala wa Yohana kwa kusoma 1 Yohana 3:11. Jiweke kwenye hali ya kwamba nimekupa kanuni moja: “mpendane.” Unaweza kujua namna ya kuishi?

1. Waweza kukabili tatizo kwa kuchukulia upendo (nia/mtazamo) na kuubadilisha kuwa tendo halisi?

2. Miaka kadhaa iliyopita nilitetea Uhuru wa dini wa waumini wa uchawi - wiccans Hilo lilinifundisha kwamba waumini wa dini hiyo wana kanuni moja kuu (the Wiccan Rede) ambayo kimsingi inasema kuwa “Fanya kile unachotaka maadam tu haumdhuru mtu yeyote.” Je, hiyo ni sawa na kuwapenda wengine? (Ningeshukuru kama kila mmoja angefuata kanuni kwamba hawatanidhuru, lakini hitaji la upendo ni matendo zaidi kuliko nadharia).

B. Soma 1 Yohana 3:12. Yohana sasa anatupatia mfano (shauri) kinyume na kanuni. Ni tafsiri gani ya upendo unayoipata kutokana na hili? (Inaonekana kama ile ya Wiccan Rede-Usiue mtu yeyote.)

1. Je, hicho ndio kipimo? Tunawapenda wengine kama tutajizuia/tutaepuka kuwaua?

2. Gundua kwamba Yohana anaandika kuhusu mitazamo/nia za Kaini. Kwa nini Biblia inajadili nia ya Kaini ya kuua? (Badala ya kubainisha kwa hakika nia za Kaini, Yohana anahusianisha matendo yake maovu na mauaji.)

a. Ni matendo gani maovu kwa upande wa Kaini yalileteleza mauaji? (Kutomtii Mungu).

b. Tumeachiwa kutafakari sisi wenyewe mitazamo tarajali. Unafikiri ilikuwa ni ipi? (Wivu dhidi ya Habili na kumwonea wivu Habili kwa kuwa alisimama na Mungu)

c. Kwa nini hilo lilileteleza Mauaji? (Nia za kiovu hupelekea kuwa na matendo maovu ambayo hupelekea mauaji. Wazo ni kwamba dhambi ni endelevu.)

d. Je, kujizuia na mauaji ndicho kipimo cha Yohana cha Upendo? (Hapana. Kwa kuangalia shauri badala ya kanuni, tunaona kwamba mfano wa jambo hasi la Yohana unasheheni katika somo kuhusu nia/mitazamo na asili ya dhambi.)

C. Soma 1 Yohana 3:13. Je, Kaini ni mfano wa jambo hasi kwetu, au ni mfano unaowakilisha dunia? (Kwa kiwango cha chini kabisa, Yohana anatuonyesha kile kisichomaanisha upendo. Siyo mauaji. Anaendelea kusema kuwa mtazamo wa dunia ni chuki, na chuki huleteleza kifo. Unaweza kutarajia dunia kukuchukia.)

1. Hebu tufanye hili kuwa la kawaida. “Wachukiaji” ni neno linalotumiwa na mashoga kuelezea Wakristo wanaoamini kwamba Biblia inazungumzia kuhusu ushoga Bango la kawaida la “mashoga” linasema kuwa “Chuki siyo maadili ya kifamilia.” Je, wana mantiki fulani hapo? Au, ni sehemu ya machukizo ya dunia kwa Wakristo iliyoakisiwa kwao kutuita wachukiaji?

2. Je, Yohana anaandika kuhusu upendo kwa Wakristo wenzetu? (Nadhani.)

a. Je, hilo linafanya suala hili kuwa jepesi? Tunaambiwa kuwapenda wale wanaojiheshimu? (Mahusiano yetu na mashoga yamefanywa kuwa magumu kwa sababu tunasema tabia yao ni ya kidhambi na wao wanaona kuwa ni mambo ya kawaida. Lakini, hata pale tunapojihusisha na Wakristo wenzetu tuna tatizo bado kwa kuwa nao ni wadhambi).

D. Soma 1 Yohana 3:14-15. Yohana anatupatia jaribu gani kujua kwamba tupo kwenye njia sahihi kuelekea nuruni? (Tunawapenda ndugu zetu. Je, tunapiga hatua yoyote hapa? Tumerejea kutafakari kile ambacho “upendo” humaanisha pale tunapojaribu kuubadili kuwa vitendo.)

1. Soma Mathayo 5:21-22. Yesu anasema “hasira=Kitu kama mauaji.” Awali hilo halionekani kuleta mantiki. Je, Yohana anaelezea kauli ya Yesu? (Nadhani hapa Yohana anaendeleza mantiki ileile. Hasira huleteleza chuki ambayo nayo huleteleza mauaji. Usiwe na hasira na kamwe hutaua. Kama ukifanya upendo usimame badala ya/mahali pa hasira basi upo katika njia ya kuelekea nuruni.)

2. Je, tuna viashiria vyovyote vya msingi vya kupima upendo wetu? (Ndiyo. Hasira siyo upendo. Chuki siyo upendo. Mauaji siyo upendo.)

E. Soma 1 Yohana 3:16. Sasa tunapata mfano wa jambo chanya. Upendo ni nini? (Kujitoa maisha yako kwa ajili ya mtu mwingine.)

1. Je, uko tayari kujitoa maisha yako kwa ajili ya Wakristo wenzako? (Kwa hakika ilikuwa rahisi zaidi pale ambapo tu nilipopaswa kuzuia mauaji!)

2. Je, mjadala wa utoaji mimba unaamuliwa vipi katika muktadha wa hii kanuni ya msingi? (Utoaji mimba ni kuyatoa maisha ya mtu mwingine kwa ajili ya manufaa yetu. Mfano wa Yesu ni kinyume kabisa: kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya mtu mwingine).

3. Utoaji mimba ni wito rahisi wa kimantiki pale unapopimwa na mfano wa Yesu. Ni vipi kuhusu nyanja nyingine za maisha, kama vile muda na fedha. Je, uko tayari kuyaacha haya kwa ajili ya Wakristo wengine?

F. Soma 1 Yohana 3:17. Yohana anasema nini kuhusu upendo na kuwasaidia Wakristo wenzetu walio wahitaji? (Anasema kuwasaidia kunaendana na mantiki ya Yesu kuyatoa maisha yake kwa ajili yetu.)

1. Kwa nini inaleta mantiki kumsaidia mtu fulani kama Yesu alitupa mfano wa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya wengine? (Utatoa nini kwa ajili ya maisha yako? Chochote kile kiwacho, kukitoa si vigumu sana kuliko kuyatoa maisha yako.)

G. Soma 1 Yohana 3:18. Yohana anamaanisha nini pale anaposema kupenda “kwa kweli.” (Hata hivyo kufanya jambo kumsaidia mtu fulani huonyesha kwamba unawapenda. Maongezi yanaweza yasiashirie ukweli wowote kabisa.)

H. Chukulia pale tulipofikia. Mfano mbovu wa Kaini unatuambia tusiue, kuchukia au kukasirika. Kuzuia mauaji na chuki inaonekana kuwa ni rahisi sana . Agano la Kale limejawa na kulaaniwa kwa matajiri wanaopora na kuwadhulumu masikini. Hiyo inaonekana kuleta maana/mantiki. Mjadala wetu hadi sasa ni himaya ya “kanuni ya waumini katika dini za uchawi”. Usiwadhuru wengine. Lakini sasa tunaambiwa kuwa tunatakiwa kutoa vitu vyetu kwa ajili ya Wakristo wahitaji. Kwa nini hili ni gumu sana ? (Tu wabinafsi. Siyo kwamba tu hatutaki kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya wengine, hatutaki kutoa vitu vyetu. Tunasema: hebu nao wajishughulishe kutafuta vyao!”.

1. Je, kuna tumaini lolote kwa ajili yetu? (Ndiyo. Hiki ndicho kikubwa kujifunza kuhusu neema, njia (njia ya Yohana ya kuelekea nuruni), na sasa rejea za maamuzi ya mashauri yaliyopita. Kwanza, tumeokolewa kwa neema (1 Yohana 2:1-2). Waliookolewa wapo kwenye njia tofauti na mashauri mabovu ya kaini wakielekea katika shauri jema la yesu.) Tunapaswa kuacha nyuma mauaji, chuki na hasira, na mitazamo yetu iwekwe katika mfano wa Yesu. Mfano wake ndilo lengo letu.)

  1. Matatizo ya Moyo
    1. Soma 1 Yohana 3:19-20. Unadhani Yohana anamaanisha nini pale anapoandika kuhusu dhamira zetu kutushitaki? Je, moyo wako umewahi kukuhukumu? (Hili ndilo jukumu la Shetani na wasaidizi wake-kutushitaki)(Ufunuo 12:10).)
      1. Tunawezaje kutofautisha shutuma za Shetani na uhukumu/uhakiki wa Roho Mtakatifu? (Mungu hutusamehe dhambi zetu tulizozitubu, lakini Shetani anakuwa anaendelea kuzileta mbele yetu ili kutukatisha tamaa. Nafikiri Yohana anasema kuwa kama ukijichunguza matendo yako, na kuona kwamba unapiga hatua mbele kuelekea kwenye mfano wa Yesu wa Upendo, basi unaweza kujiamini kuwa upo kwenye njia yenye nuru. Una “uthibitisho” kuwa maisha yako yanaelekea kwenye uelekeo sahihi.)
    2. Soma 1 Yohana 3:21-22. Kwa nini Yohana tena anarejea habari za kupokea kitu fulani/chochote? Nilidhani tumekubaliana hivi punde tu kwamba tunahitajika kuwapatia vitu wale Wakristo walio wahitaji. (Picha yote sasa imefunuliwa-kama Yesu alikuwa radhi kutupatia maisha/uhai wake, yuko radhi kutupatia vitu. Yohana anafundisha kwamba kama tukiifungua mioyo yetu (na pochi zetu) kwa wale walio wahitaji, Mungu atafungua pochi yake kwetu.)
    3. Soma 1 Yohana 3:23-24. Baada ya huu mjadala kuhusu kuwasaidia wengine, kwa nini Yohana anasema “amri yake” ni “kuliamini jina la Mwana wake?” ( Kama tulivyojadili, Yesu ndiye mfano wa mwisho wa kujitoa kwa ajili ya wengine. Yesu pia ni mfano wa mwisho wa kujitoa kwa ajili ya wengine. Yesu pia ni mfano wa mwisho wa kuheshimiwa kwa ajili ya hili.)
    4. Rafiki, vipi kuhusu wewe? Utadhamiria leo kwamba utawasaidia Wakristo wenzako walio wahitaji? Utagawana nao muda wako na vitu vyako pamoja nao?
  2. Juma Lijalo: Kumwamini Mwana wa Mungu.

Tuesday, August 11, 2009

CALAMITIES

In the face of what we hear every day in the news, on what we read on papers and on what we do witness around us (wherever you are) we surely realise that nothing can be far from the truth, we are living on the last days, and the Lord's coming is nigh. Below is the extract from the book of LAST DAYS EVENTS written by the servant of the Lord sister Ellen. G. White.


 

LAST DAYS EVENTS - CHAPTER FOURTEEN

- Calamities -

Manuscript 127, November 22, 1897, (see also 3SM 311-12; UL 340) 

The Lord is teaching men that there are limits to His forbearance. In fires, in floods, in earthquakes, in the fury of the great deep, in calamities by sea and land, the warning is given that God's Spirit will not always strive with men. The times in which we live are times of great depravity and crime of every degree. Why?--because men, whom God has blessed and favored, have reduced His holy law to a dead letter, making void the law of God by the traditions and inventions of the man of sin....

 It is a terrible thing for a nation to wear out the patience of God. Each century of profligacy has treasured up wrath for its iniquity against the day of wrath. Christ is now bidding the abandoned of our day to fill up the measure of their fathers in their iniquity. When that time shall come, and their cup of iniquity is filled up, it will be demonstrated that to wear out the patience of God brings tremendous consequences to the disobedient. The nations of earth will act upon a shortsighted policy. Through their own course of action the priests and rulers will restore the lost ascendancy of the man of sin.

 Behold Satan's miracle-working power. Every object in the earth, in the air, and in the water has been employed to confirm his claims. Those who yield to these claims are alive with intense activity, one influencing and stimulating another by confirming the greatness and glory of their kingdom. See the activity, the restless surging of the masses in their determination to take and occupy the place of the throne of God. What eagerness, what rage they exhibit in their religious enthusiasm. Mark the defiant rebellion written in their countenances. Their warfare is against their Creator and Redeemer. How vast is the procession they form! How mighty they think themselves to be in their countless numbers.


 

Letter 21, February 16, 1902, (see also CM 19-20)

     Is it true that the end of all things is at hand? What mean the awful calamities by sea--vessels shipwrecked and lives hurled into eternity without a moment's warning? What mean the awful accidents by land--fire consuming the riches men have hoarded, much of which has been accumulated by oppression of the poor? The Lord will not interfere to protect the property of those who transgress His law, break His covenant, and trample upon His Sabbath, accepting in its place a spurious rest day. As Nebuchadnezzar set up an image in the plains of Dura, and commanded all to bow before it, so this false sabbath has been exalted before the world, and men are commanded to keep it holy....

     The plagues of God are already falling upon the earth, sweeping away costly structures as if by a breath of fire from heaven. Will not these judgments bring professing Christians to their senses? God permits them to come that the world may take heed, that sinners may be afraid and tremble before Him.


 

Letter 12, December 23, 1909, (see also 7ABC 123-24; 1MCP 40-42)

     Calamities are becoming more and more common, but every report of calamity by sea or by land is a testimony of the fact that the end of all things is near. The world is filled with iniquity, and the Lord is punishing [the world] for its wickedness. As crime and iniquity increase, these judgments will become more frequent and more marked, until the time shall come when the "earth...shall no more cover her slain" [Isaiah 26:21].

Monday, August 3, 2009

Somo la 6: Kutembea Nuruni: Kuwakataa Wapinga Kristo

(1 John 2:18-29, 2 Corinthians 1)

1, 2 & 3 Yohana: Somo la 6


Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sememu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kizulu, nk.



Utangulizi: Wiki iliyopita tulijifunza kuwa watu werevu walikuwa na matazamio ya masuala ya umilele na utajiri wa milele. Kwa nini ni waerevu kufanya hivi? Kwa sababu dunia hii itaishia kuungua wakati ambapo wale walio na mtazamo wa kimbingu watakuwa na uzima wa milele wakifurahia hazina za milele. Mtazao huo hugawanya "walio wa kidunia" kutoka kwa wale waaminio. Wiki hii Yohana anageukia uzingativu wake kwenye tatizo lisilokuwa la kawaida. Anatuonya kuhusu "wapinga Kristo." Hebu tujitose kwenye kwenye ujifunzaji wetu wa Biblia na kubaini kuhusu hawa  wapinga Kristo na jinsi ya kujizuia kutumbukia katika tatizo la upinga Kristo!


 


 

  1. Saa ya Mwisho


     

    1. Soma 1 Yohana 2:18. Hawa "watoto" ni akina nani? (1 Yohana 2:1 ilianza kwa kauli hiyo hiyo, "watoto wangu." Tuliamua hapo kabla kuwa hawa ni wafuasi wa Yesu. Kumbuka kutoka wiki iliyopita kwamba "watoto," kinyume na "akina baba" au "vijana" (Tazama 1 Yohana 2:12-14), inawarejea waumini wapya. Hawa ni watu ambao wana mengi ya kujifunza.)


       

      1. "Saa ya mwisho." Yohana anamanisha nini katika hili? Saa ya mwisho ya historia ya dunia?


         

      2. Soma Kumbukumbu la Torati 18:20-22. Kama Yohana anamaanisha kuwaambia wasomaji wake mwisho wa wakati umekaribia, je, hiyo hufunua kuwa yeye ni nabii wa uongo na kwamba tuache mara moja kusoma barua zake?


 

  1. Umesikia "mwisho wa wakati," "zama za mwisho," "siku za mwisho" na kauli kama hizo. "Saa ya mwisho" inaonekana kuwa mwisho wa miisho, sawa?


 

  1. Soma Mathayo 24:30-34. Yesu anasema nini: kwamba wale waliokuwa wakimsikiliza hapo awali watauona ujio wake wa mara ya pili?


     

    1. Kama ndivyo, je, Yohana alikuwa anarudia tu kitu kisicho sahihi ambacho Yesu alikisema?


       

    2. Kwa kuwa hatuwezi kumpigia kura Yesu kama nabii wa uongo, tuupigie kura Ukristo wote?


 

  1. Soma Mathayo 24:1-3? Unafikiria nini juu ya ubora wa swali la faragha la wanafunzi?
    1. Tatizo limeunganishwa? (Ndiyo. Wanafunzi wanauliza kuhusu uharibifu wa hekalu na mwisho wa dunia. Waliamini kimakosa kwamba matukio hayo mawili yalikuwa ni tukio moja.)


       

    2. Yesu anajadili swali lipi? (Uharibifu wa hekalu Yerusalemu. Hili lilitendeka mwaka 70 BK. Kama Yesu bado anaongelea kuhusu ule uharibifu, kauli ya "kizazi hiki" ni ya kweli.


     

    1. Yesu anaonekana kuunganisha Ujio Wake wa Mara ya Pili na uharibifu wa hekalu. Je, huu ni "usaidizi wa upotoshaji," "uongo wenye manufaa" (ili tusikatishwe tamaa), au kuna kitu kingine kinaendelea? Je, kauli ya Yesu ni kitu ambacho kinatusaidia kuelewa "saa ya mwisho" ya Yohana? (Jiweke katika viatu vya wasikilizaji.. Hekalu ndilo lililokuwa kitovu cha kuabudu kuliopo. Mfumo wa kuabudu wa hekalu ulikuwa ni ishara ya kifo cha Yesu, maisha na kutuombea dhambi zetu. Uharibifu wa hekalu muda mfupi baada ya Yesu kusulubiwa ulianzisha ukurasa mpya kwa wafuasi wa Mungu-siku za mwisho, mwisho wa zama, saa ya mwisho.)


       

      1. Je hii inaweza kuwa ni sababu kuwa wanafunzi hawakuweza kufikiri dunia bila ya hekalu? (Ndiyo. Kama mfumo wa ibada kwa Mungu wa ukweli ungetoweka, ingemaanisha Mungu hakuwa tena akiuongoza. Hiyo isingewezekana. Wanafunzi hawakuweza kuelewa bado kuwa Yesu ndiyo alikuwa sababu mfumo wa kafara ukawepo.)



  1. Mpinga kristo


     

    1. Hebu na tuendelee mbele na 1    Yoh 2:18. Ni kwa jinsi gani makristo wa uwongo wanahusika na saa ya mwisho? ( Haya machafuko katika mfumo wa ibada unatoa fursa kwa walimu wa uwongo.)


 

  1. Je ni wapinga kristo wangapi tulio nao? (Inaonekana ni wengi)\
  2. Je unafikiri Yohana anamaanisha nini kwa neon "mpinga kristo" na "wapinga kristo wengi?" (Inaonekana yupo mpinga kristo mkuu. Lakini yaonekana wapo wapinga kristo wengine wadogo pia.)


 

  1.   Mpinga kristo ni neon tete. Hebu tusome 1 Yohana 2:19-22 kupata picha hasa ya nini neon hilo humaanisha.


     

    1. Je wapinga kristo ni watu waliokuwa wazuri awali wkitembea katika nuru? ( Walihusiana na kundi la waaminio. Yohana anasema kuondoka kwao kunaonyesha kuwa hawakuwahi kamwe kuwa sehemu ya kundi. Japo, walionekana kuwa sehemu ya kundi.)


       

    2. Ni njia ipi ya awali kabisa ya kumtambua mpinga kristo? (Yeye asemaye uwongo juu ya kweli. Ukweli wa msingi ukiwa ni kuwa Yesu ni Mungu. Ukikataa ya kwamba Yesu si Bwana, utakuwa unamkataa Mungu baba pia.)


 

  1. Ni kwa jinsi gani hiyo ni ukweli? Ni kwa jinsi gani hatukuweza kuamini katika "Mungu mmoja (kama ilicyo kwa Wayahudi na Waislamu) wa agano la akale bila kukuibaliana na huu wingi wa Mungu ambao wakristo wanautangaza ? (Kama hukufahamu kwambaYesu ndiyo alikuwa sababu kwa mpango wa hekalu wa Mungu wa ondoleo la dhambi, kivyovyote hutoweza kuelewa ukweli ao kuweza kuelezea ukweli juu ya Mungu. Katika mwaka 70 A.D. saa ya mwisho ilifika ambapo watu aidha walielewa mpango wa Mungu na kufanya mabadiliko kutoka huduma za ishara na kumtazama Yesu, au waliachwa nyuma katika ujinga.)


 


 


 

Soma 1Yohana 2:23. Je hii inaleta mantiki kwako? (Kama kukmubali Yesu na kafara yake ni njia mpaaya iliyoainishwa ya kuondokana na dhambi, hivyo itakuwa ndiyo njia pekee ya kumwendea Mtakatifu Mungu Baba.)   


 

  1.  Soma 1Yohana 2:24-25. Nini uhusiano kati ya uzima wa milele na Yesu? (Kwa kuwa kifo cha Yesu kwa niaba yetu (tulikuwa na Yesu pale naye alipofariki) ndiyo ufunguo wa ondoleo letu la dhambi, kifo chake pia ni ufunguo kwa maisha yetu ya umilele!)


 

   
 

  1. Kupakwa mafuta


     

    1. Tumejifunza kwamba ni muhimu kuhifadhi " kile tulichosikia tangu mwanzo" (1 Yoh 2:24). Ni nini kinachofanya ukweli udumu? (soma tena 1 Yohana 2:20: kutawazwa na Mtakatifu.")


     

    1. Mtakatifu iatakuwa inazungumzia Mungu. Kupakwa gani mafuta huku kuliko kwa muhimu?


 

  1. Soma 2 Wakorintho 1:21-22. Fungu hili huelezeaje upakwaji wa mafuta?


 

  1. Tunafahamu jinsi ya kulipia kitu mapema kidogo kwa kiasi (deposit) kwa kitu tutakachonunua. Ni kwa jinsi gani roho mtakatifu ni deposit kwa ujio wa Yesu mara ya pili? Ni kwa jinsi gani roho mtakatifu ni deposit inayotufanya tuendelee kuamini katika Yesu? (Deposit ni sehemu ya bei ya ununuzi. Ni sampuli ya baki. Tutakapoenda mbinguni wakati wa ujio wa Yesu mara ya pili tutaishi katika uwepo wa Mungu. Tunaweza kuanza kuelewa sasa hivi ni kwa vipi tutaishi mbele ya uwepo wa Mungu wakati tukiwa tumejawana roho mtakatifu.)


     

  1. Hofu yako kubwa ni ipi katika kumwamini kwako Mungu?( kwamba tunaamini kitu ambacho siyo kweli. Kwa kawaida huwa nasoma vitabu maarufu vya kisayansi na jambo kubwa mara nyingi ni kuwa hakuna Mungu, ila palitokea uibikaji (evolution))

    1. Ni kwa jinsi gani Roho Mtakatifu anatupa uthibitisho wa uwepo wa Mungu? (Kama unajua Roho Mtakatifu anafanya kazi katika maisha yako basi unauthibitisho ya kuwa Mungu yupo na kwamba Biblia ni ya kweli.)


 

  1. Soma Yohana 16:13. Ni kwa jinsi gani Roho Mtakatifu aweza kutuongoza katika kuujua ukweli kuhusu Mungu? (Mara nyingine huwa nashangaa sana ni kwa jinsi gani hawa wanasayansi wanaweza kuwa wapumbavu. Wanaandika vitabu juu ya kanunni zinazosimamia mfumo wa uumbaji. Wanaafiki ya kwamba wanfahamu kanuni nyingi kupitia vipimo –hawafahamu mantiki ama sababu zinazozunguka kanuni. Wakati katika ulimwengu huu wenye kujali usahihi, kanuni wanaaamini ya kwamba kila kitu kilitokea kwa bahati! Roho mtakatifu anatupa fikra safi na thabiti ya upungufu katika kfumo huo wa fikra.)


 

  1. Soma 1 Yohana 2:-26-27. Je hii humaanisha kwamba hunihitaji mimi? Huhitaji mwongozo wa kujifunza Biblia? Hatuhitaji nyaraka za Yohana? (Nafikiri Yohana anasema kuwa hatuhitaji walimu wa uwongo. Kama ambavyo unaweza ukawa umeshabaini, jinsi navyoandaa masomo haya ni katika mtindo ambao utakufanya usome Biblia, na kasha kukuuliza maswali juu ya kile ulichokisoma. Lengo langu ni kukusaidia ufikiri juu ya neon la Mungu na kumwacha Roho wa Bwana akuongoze.)
     

  2. Soma 1 Yohana 2:28-29. Wajib u wetu ni upi? (kuendelea kutembea katika nuru!)


 

  1. Rafiki, kama unaamini ya kuwa Yesu ni mwana wa Mungu, kama unaikubali kafara yake kwa niaba yako, basi upo katiaka njia ya kuelekea ufalme wa milele. Kama unahitaji msaada (na unauhitaji) je utamwomba roho mtakatifu akujaze?\je utaanza kupata uzoefu sasa wa kuishi mbele za Bwana? Kwa nini usiliombee hilo sasa?


 

  1. Juma lijalo: Kuishi kama watoto wa Mungu


     


     

Friday, July 24, 2009

Somo la 5:Kutembea Nuruni: Kuyakana Mambo ya Ulimwengu


(1 Yohana 2)

1, 2 & 3 Yohana: Somo la 5

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sememu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kizulu, nk.

Utangulizi: Kuishi pembezoni mwa bahari inamaanisha kuwa natumia muda mwingi ufukweni kuliko nilivyokuwa nafanya huko nyuma. Mara kwa mara nawaona wanawake wa kiislam wakiwa ufukweni. Tofauti kati yao na watu wengine wa kawaida wanaotembelea ufukweni ni dhahiri. Inanikumbusha nilipokuwa kijana na washiriki wa kanisani kwangu walikuja siku ya Sabato karibu na fukwe za karibu za Ziwa Michigan. Mara kwa mara washiriki wa kanisa bado walikuwa wakivaa suti na mavazi ya kikanisa, wakati ambapo watu waliokuwa wakiota jua walikuwa vakivaa vitu tofauti kabisa. Somo letu la juma hili ni kuhusu "mambo ya ulimwengu." Je, mifano hii miwili ni ya kuyakana "mambo ya ulimwengu"? Is sticking out like a sore thumb God's goal for us? Au, hiyo ni kuifanya kauli ya wazi kwa ulimwengu? Hebu tujivinjari kwenye somo letu la Biblia na kuona kile ambacho Yohana anatufundisha kuhusu mambo ya ulimwengu!

  1. Watoto, Wanaume na Akina Baba
    1. Soma 1 Yohana 2:12-13. Yohana anasema anawaandikia watoto, akina baba na vijana. Je, hiyo ndiyo sababu tuna nyaraka tatu: Yohana wa kwanza, pili na tatu?
      1. Kama ndio hivyo, kwa nini Yohana anaonyesha makundi mengine mawili katika Yohana wa Kwanza? (Yohana hana waraka mwingine kwa kila kundi.)
      2. Je, Yohana ana ujumbe wa aina tatu tofauti kutegemeana na kundi linaloelezewa?
      3. Kwa nini wanawake wameachwa, yaani, hawakutajwa kwenye ujumbe? Je, wao tayari ni wenye haki?
    2. Hebu kwanza tuwaangalie watoto. Fungu linasema kwamba wamesamehewa dhambi zao na kwamba wamemjua baba. Je, hilo siyo kweli pia kwa makundi yote matatu? (Nafikiri Yohana anazungumzia waumini wapya, siyo watoto kikwelikweli. Muumini mpya anaweza asiwe na uelewa mpana wa injili. Hata hivyo muumini mpya ambaye alikuwa Myahudi aliyebadili dini ange "mjua Baba," ikimaanisha Mungu wa Agano la Kale. Muumini mpya angekuwa katika jukwaa la uelewa kwamba Yesu alikuwa kafara "mpya" ya dhambi. Sababu ambayo Yohana hawataji wanawake ni kwamba anaandika kuhusu kukomaa kiroho, siyo jinsia.)
    3. Tuna ujumbe gani kwa akina baba-Wakristo waliokomaa? ("Umemjua Yeye ambaye yupo tangu mwanzo.")
      1. Unadhani hili linamaanisha nini? (Kama tulivyoona hapo awali, hili linamrejea Yesu (Yohana 1 na 1 Yohana 1). Hawa ni Wakristo walio na uelewa wa Yesu.)
    4. Tuna ujumbe gani kwa "vijana?" (Wamemshinda mwovu.)
      1. Tunawezaje kusema kwamba mwanadamu yeyote "anamshinda mwovu?" (Hawa ni Wakristo wanaokua. Wanatambua kwamba Yesu amewasamehe dhambi, lakini wana mwendo wa kiroho kuelekea kwenye haki. Wanaweka lengo la kila siku la utii.)
    5. Soma 1 Yohana 2:14. Ni kitu gani kingine tunachojifunza kuhusu "vijana?" (Neno la Mungu hukaa ndani yao. Wanasoma neno la Mungu. Wanamtegemea Roho Mtakatifu.)
    6. Hebu tufanye tathmini: Yohana anawaandikia waumini wa madaraja yote ya ukomavu wa Kikristo. Anasifia  kila kundi katika maendeleo waliyoyafikia hadi sasa. Kinachofuata, tunageukia ujumbe wake kwa makundi yote.
  2. Kuipenda Dunia
    1. Soma 1 Yohana 2:15. Kila kitu ninachokijua na kukigusa na nilichokizoea kipo "duniani". Nawezaje nisikipende?
      1. Kwa kuwa tumeambiwa kuwa kuipenda dunia ni kinyume na kumpenda Mungu, unadhani inamaanisha nini kusema kuwa "dunia" na "chochote kilichomo duniani?"
    2. Soma 1 Yohana 2:16. Tunaona nini "duniani?" (uchu, tamaa ya mwili na kujisifu/kujigamba.)
      1. Je, "mambo" haya yamo "duniani?" (Hapana. Hii ni mitazamo kuhusu vitu fulani.)
      2. Hebu tuangalie hili kidogo. Kama Yohana anaongelea kuhusu mambo ya ulimwengu, je, anatufundisha kwamba mambo ya ulimwengu ni mtazamo au matarajio?
        1. Kama habari ndiyo hiyo, kuna uhusiano gani kati ya jinsi Mkristo anavyovyaa na mtizamo wa Mkristo?
          1. Hili linasema nini kuhusu "vazi la ufukweni" nililolielezea kwenye utangulizi? Je, kujivika, au kuvaa mavazi tofauti, ni kukataa/kukana mambo ya ulimwengu?
      3. Kama uchu, tamaa ya mwili na kujisifu/kujigamba ni mitizamo kuhusu vitu fulani, je, hiyo inamaanisha kuwa watu wasio na vitu (masikini) wanaweza kuwa wa dunia? (Kinyume chake ni kwamba wale wasio na vitu wanaweza kuwa na matatizo mengi kuhusiana na hili kuliko wale walio na vitu na kuamua kuwa "vitu" siyo vya msingi kihivyo.)
    3. Soma tena 1 Yohana 2:16. Kauli "cravings of sinful man," inatafsiriwa kuwa "tamaa ya mwili."  Hii inatusaidiaje kujua kile inachomaanisha? (Mtu aliye na tamaa hizi (hii "tamaa") ana mtazamo juu ya mambo ya kidunia.)
      1. Vipi kuhusu wewe? Una mtazamo wa kidunia? Unatamani vitu fulani? Unatamani ungekuwa na vitu fulani?
    4. Tulipokuwa tukielekea kanisani wiki iliyopita, mimi na mke wangu tulikuwa tukiongelea mambo ya mbeleni. Tunapanga kuuza nyumba yetu ya sasa na tulikuwa tunajadili kuhusu mahala pengine pazuri/bora pa kuishi. Mahala pazuri kwangu ni nyumba hii (hapa tunapotaka kupauza) karibu kabisa na ufukwe ambapo unaangalia ghuba ya Chesapeake na bahari ya Atlantiki. Gharama? Dola milioni 1.3. mke wangu angependa kuishi katika milima ya  Blue Ridge-takriban saa 3 kutoka ufukweni. Nikasema, "Kama tungekuwa na pesa za ziada kidogo tungejipanga"-ikimaanisha kwamba tungeweza kununua nyumba ya ufukweni na nyumba iliyopo katika milima ya Blue Ridge . Je, hizo ni "tamaa za mdhambi" na "tamaa za macho yake?" (Ndiyo! Angalao kama inaelekea kwenye hatua ya uchu na kutamani tofauti na kuchukulia kwamba mambo haya hayawezekani.)
    5. 1 Yohana 2:16 inamaanisha nini inaporejea "tamaa ya macho yake?" (Unataka kile unachokiona.)
      1. Kwa nini hili ni makosa? (Vitu vya kiroho kwa ujumla huwa havionekani. Vitu vya kiroho mara kwa mara huwa ni mahusiano. Kwa hiyo, unatamani juu ya mambo mabaya/yasiyostahili katika maisha.)
    6. 1 John 2:16 inarejea kitu gani inapoongelea "kusaidia kile alichonacho na akifanyacho?" (Huu ni mshale moyoni mwangu. Mara zote nimekuwa nikifurahia kuwa mwanasheria. Napenda kusema kuwa mimi ni mwalimu wa shule ya sheria kwa sababu inapendekeza kuwa mimi siyo mwanasheria tu, bali mwanasheria mwerevu. Hili ndilo linaonekana kwa hakika Yohana analishutumu kuwa la kidunia. Kama mtu yeyote anataka kuniokoa kwa kupendekeza tafsiri nyingine, nipo wazi kulisikiloiza! Kwa sasa ninatubu.)
  3. Mtazamo wa mbali
    1. Soma 1 Yohana 2:17. Kuna shida gani na aina hizo za matamanio? Haya mambo ya ulimwengu?
      1. Je, Yohana anasema kwamba mtazamo wa kidunia, kuwa na hisia kuhusu kuwa na "vitu" ni dhambi? Au tu ni kujishughulisha/kujifikirisha kipumbavu?
      2. Kama mtu hampendi Mungu, je, hiyo siyo ishara ya "dhambi?" (Yote haya yana mantiki kwangu. Kama tunajishughulisha na kupata vitu, basi hatujishughulishi na kumjua Mungu. Mathayo 6:24 inasema kwamba fedha ni bwana. Hatuwezi panda na kumtumikia Mungu na pesa. We cannot love and serve both God and money.)
      3. Umewahi kusikia msemo "ilikuwa nzuri wakati ambapo ilikaa kwa muda mrefu?" Je, linahusika hapa-kwenye kauli ya 1 Yohana 2:17? 
      4. Mungu anatupatia kitu gani kilicho bora sana? (Uzima wa milele! Vitu vya milele. Nadhani Yohana anajenga hoja kivitendo. Kile ulicho nacho na vile jinsi ulivyo sasa ni vya muda tu. Pale unapokufa, nani anakumbuka au anajali? Pesa yako inakwenda kwa mtu mwingine. Inaleta mantiki gani kujishughulisha na kitu ambacho kwa hakika utakipoteza? Kwa upande mwingine, Mungu anatupatia vitu vya milele na sifa njema.)
    2. Una ufahamu wa kiasi gani kuhusu babu zako wa mbali sana (mababu wa babu zako)? (Nilipokuwa ninaandika somo hili, mke wangu alipata na kunitumia kipande cha picha ya video kuhusu kujiuzulu kwa baba yangu katika wadhifa wake wa mwisho. Kitini hicho kilikuwa na kichwa cha habari kikubwa na picha ikionyesha kwamba baba yangu alikuwa mtu mzuri sana wa sura. Lakini kitini hicho ni kama vile hakikuelezea chochote kuhusu kazi yake au mafanikio yake. Badala yake, kilitaarifu kuwa alikuwa na ugonjwa wa moyo, kikaonyesha kiasi alichopata (pesa) na kwamba walikuwa watafuta mtu mbadala. Kile tulichonacho na kile tunachokifanya, yote ni ya muda tu!)
    3. Rafiki, vipi kukuhusu wewe? Unatizamia umilele au mambo ya dunia hii? Kwa nini usiamue leo kutizamia kwenye mambo ambayo hayataisha kamwe! Habari gani kuhusu kuwa wa "kimbingu" badala yaw a "kidunia?"
  4. Wiki Ijayo: Kutembea Nuruni: Kuwakataa Wapinga Kristo.


 

Kama ilivyofasiriwa na Mgune Masatu.

Friday, July 17, 2009

Somo la 4: Kutembea Nuruni: Kutunza Amri Zake

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sememu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kizulu, nk. Muombe Roho Mtakatifu akuongoze ujifunzapo somo hili.

 
 

Utangulizi: Mojawapo ya majukumu yangu kama mwanasheria ni kuthibitisha mada za kesi za wateja wangu. Ninapokuwa nikitetea kesi za kidini, kitu cha kwanza ni kuthibitisha kwamba mteja wangu ana "imani ya kidini ya dhati." Wewe ungefanyaje kuhusiana na hilo ? Utathibitishaje kwa hakimu, asiyemfahamu mteja wako, kile kilichomo moyoni mwa mteja wako? Ninatumia matendo ya mteja wangu kuthibitisha kile kilichomo moyoni mwake. Je, njia yangu ni njia ya Mungu? Matendo yetu yana uhusiano gani na kile kilichomo mioyoni mwetu? Hebu tujivinjari kwenye somo letu na kubaini kile ambacho Mungu anakisema kuhusu hili!


 

  1. Lengo
    1. Soma 1 Yohana 2:1. Wiki iliyopita tulijifunza kwamba wale "wanaotembea katika nuru" wana dhambi maishani mwao. (1 John 1:7-8) Je, hilo linakanusha matendo yangu = nadaharia ya moyo (heart theory)?
      1. Je, dhambi hiyo ni sawa tu kwa Yohana? Ni vipi kuhusiana na hilo kwa Mungu? Je, ni sahihi kutembea katika njia ya nuru ukiambatana na mzigo huu wa dhambi?
      2. Yohana anasema kuwa lengo ni nini? (1 Yohana 2:1: "Nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi." Lengo ni kuachana na dhambi.)
      3. Je, hili ni lengo halisi? Nini kinatokea endapo tutakosea? (Yohana anasema kuwa tunaye Yesu mtetezi wetu. Inafanana kabisa/Yesu anaonekana kama mwanasheria!)
    2. Angalia tena 1 Yohana 2:1. Yesu "anatuteteaje" mbele za Baba? Kwa kujenga hoja kwamba kila mtu anatenda dhambi, na kwamba Mungu asiangalie dhambi mojamoja?
      1. Je, Yesu anajenga hoja kwamba kile tulichokifanya hakikuwa dhambi haswa?
    3. Soma 1 Yohana 1:10. Ni watu wa aina gani tulioamua wiki iliyopita kuwa ndio walioelezewa hapa? (Haya ni makundi mawili: Kwanza, wale wanaodai kuwa wamefikia kiwango cha ukamilifu na kwamba hawana dhambi. Pili, wale wanaosema kuwa hawatendi dhambi sasa na kamwe hawajawahi kutenda dhambi kwa sababu dhambi kwa hakika haipo kwa ajili ya Wakristo. Inaleta mantiki kwamba Yesu asingekuwa anarudia kubadilika kwa hizi hoja mbili potofu.)
    4. Unafikiri watu walioelezewa katika 1 Yohana 1:10 ndio wale wale ambao Yohana anazungumza nao katika 1 Yohana 2:1? (Hapana. Yohana anaanza kwa kusema "watoto wangu wadogo." Haendelei kuzungumza na kundi la watu wale wale aliokuwa akiwaongelea katika fungu la 10. Alisema kuwa watu walioelezewa kwenye fungu la 10 walikuwa wanamfanya Mungu kuwa mwongo na neno la Mungu halina nafasi maishani mwao. Yohana amegeukia kundi lingine la watu wanaoutafuta ukweli. Hawa ni watu wanaotembea kwenye njia
      ya nuru. Hawa ni watu wanaotaka mioyo yao na matendo yao kushabihiana/kuendana.)

    5. Sasa kwamba tumeshajadili kile tunachofikiri Yesu anaweza kukijengea hoja, hebu tusome 1 Yohana 2:2 na kujaribu kuona kama tunaweza kubaini kile ambacho kwa hakika anakijengea hoja. Ni hoja ya aina gani inapendekezwa ambayo Yesu anaifanya badala yetu?
      1. Fikiria kwamba umeburuzwa mbele ya hakimu na unashitakiwa kwa kufanya kosa la jinai. Na pindi usimamapo na kujaribu kujiweka vizuri (na kutokuwa kwako na hatia) mara unamsikia wakili wako akianza kujenga hoja zake: "Mheshimiwa, mteja wangu ana hatia, tena ana hatia sana….." Ungesema nini?
        1. Je, huo ndio utetezi wa Yesu kwa ajili yetu? (Ndiyo! Utetezi wake ni kwamba tuna hatia sana , lakini tayari amekwishalipa adhabu. Habishani dhidi ya hatia yetu. Anabisha dhidi ya adhabu nayowekwa juu yetu.)
      2. Katika muktadha wa hoja ya Yesu (wakili wako), ni vipi juhudi zetu za kuficha na kukataa dhambi zetu zinaonekana? Fikiria hatua ya hakimu kama ungeanza kupingana na wakili wako na kauli ya kuudhi, "Sina hatia! Naishi maisha makamilifu! Matatizo yoyote ninayoweza kuwa nayo siwajibiki nayo. Ni makosa ya kurithi niliyoyapata kutoka kwa baba yangu na mama yangu!"
    6. Tumeamua dakika chache zilizopita kuwa 1 Yohana 2:1 imeelekezwa kwa "wale walio katika njia yenye nuru." Je,hili liko sawa na 1 Yohana 2:2? (Kafara ya Yesu ni "kwa ajili ya dhambi za dunia yote." Kafara yake inaweza isikubaliwe na wote, lakini aliyatoa maisha yake kwa kila mtu.)
    7. Fikiria hili: Kwa nini Yohana anamuwianisha Yesu kama anayetutetea au anayepigania nafsi yetu kwa Mungu? Je, Mungu Baba anahitaji kushawishiwa? Je, hii ni aina fulani ya mjadala ambayo tunatumai kuwa Yesu anashinda?
    8. Soma Yohana 16:26-27 ambapo Yesu anasema kuwa "wala siwaambii ya kwamba mimi nitawaombea kwa Baba; kwa maana Baba mwenyewe awapenda….." Hili linalinganaje na uhitaji wa wakili? (Utetezi wa Yesu ni kinyume na matakwa ya sheria, na siyo matakwa ya uhasama (kwetu, badala ya juu ya dhambi) ya Baba. Kile ambacho Yesu ametutendea ni zaidi ya maneno ya kuelezeka, na ukweli kwamba Yesu anajitokeza mbele kwa niaba yetu hufanya utetezi wetu kuwa dhahiri.
  2. Kumjua Mungu
    1. Soma 1 Yohana 2:3-4. Mara kwa mara mtu fulani huniuliza kama namfahamu mtu fulani muhimu. (Kwa kweli, kwa ujumla huwa ni kinyume,huwa nina shauku kuwaelezea wengine kama namfahamu mtu yeyote ambaye si wa muhimu. Ina maanisha nini "kumjua" mtu fulani? Yohana anamaanisha nini anapotuandikia sisi kuwa anamjua Yesu? (Kumjua mtu fulani inamaanisha kuwa unafahamu kitu fulani kumhusu.)
      1. Kama hili ni kweli, sasa kwa nini tena utii wa sheria ya Mungu ni "kipimo cha uhalisia" wa kumjua Mungu? (Kimantiki, lazima imaanishe kuwa kuna muunganiko thabiti kati ya kumjua Yesu na kujua amri zake.)
      2. Je, hili linathibitisha mtazamo wangu wa kimahakama: kwamba matendo ya mteja wangu yanaelekea kuonyesha endapo mteja "anamjua" Yesu? Ana moyo kwa ajili ya Yesu?
    2. Kwa nini Yohana anasema kuwa tumheshimu Yesu?  Motisha yetu ni nini? (Tunamjua.)
      1. Kwa nini Yohana hasemi tutii kwa sababu tunajua kanuni?
      2. Kwa Yohana hasemi  tutii kwa sababu tunamcha Mungu?
      3. Kwa nini Yohana hasemi  tutii kwa sababu tumepitia uzoefu wa changamoto ngumu kabisa ama uzoefu wa raha na hali njema
    3. Je, hii ni kanuni ya Ulimwengu? Ya kwamba tutii kile tunachokijua?
      1. Kama utasema, "ndiyo," jiulize kuwa ulitumia muda gani kumjua Mungu wiki iliyopita ukilinganisha na kulijua joka likiongea kupitia kwenye televisheni?  
    4. Kama utasema, "siyo kweli, Bruce, kwamba natii kila kitu ninachokijua," basi kwa nini kumjua Mungu inamaanisha kuwa tumtii? (Hii inasema chemsha bongo fulani kuhusu Mungu. Pendo lake na tabia yake ni kwamba kumjua hutufanya tutake kutii!)
    5. Marafiki zangu, hili ni jambo linaloua: hatuwezi kumtii Mungu isipokuwa kama tunamjua. Upande mwingine wa mlinganyo huu ni makini zaidi: hatumjui kama hatumtii.)
    6. Soma 1 Yohana 2:5. Unafikiri Yohana anamaanisha nini pale anaposema kuwa upendo wa Mungu umekamilika kwa yeyote yule anayetii? (Ukristo siyo wa kinadharia. Siyo uelewa wa kanuni  zinazodhanika ambazo hazileti utofauti wa kivitendo katika maisha yetu. Upendo wa Mungu unakamilika kwetu pale tunaporuhusu mapenzi yake yabadilishe matendo yetu.)
    7. Soma 1 Yohana 2:6. Inamaanisha nini "kutembea" kama Yesu alivyoenenda? Je, inamaanisha kuwa:
      1. Hatuna fedha?
      2. Hatuna mke/mume (mwenza)?
      3. Tunahubiri? (Yohana kwa hakika, kwa uwiano sahihi, anaelekeza dhana kuwa utii ni wa msingi sana . Haongelei kuhusu masuala fulani ya maisha ya Yesu, anaongelea kuhusu dhamira ya Yesu ya kumtii Baba yake na kuakisi mapenzi ya Baba yake. Mioyo yetu na matendo yetu ina uhusiano.)
  3. Matokeo ya Kumjua Mungu.
    1. Soma 1 Yohana 2:7-8. Je, Yohana anatukumbushia kuhusu amri ya zamani au anatuambia kuhusu amri mpya? Yohana anaanza kwa kile kinachoonekana kama vile ana kipingamizi: "siwaandikii amri mpya, ila amri ya zamani. Labda ni aina fulani ya amri mpya." Ni ipi hii? (Ni amri ya zamani ambayo haitambuliki kwa dhahiri hapo kabla kwa sababu mwanga mpya unaturuhusu kuiona.)
      1. Umewahi kupata kitu cha kale, ukakisafisha, na kudhani kuwa kimeonekana tofauti kabisa? Kipya kabisa?
    2. Soma 1 Yohana 2:9-11. Je, hii sheria ya kale iliyofanywa kuwa mpya ni ipi? (Kuwapenda Wakristo wenzetu).
      1. Imewezwaje kufanywa upya? Asili ya mwanga mpya ni ipi? (Hujui namna ya kupenda, Yohana anasema, hadi mmeona jinsi Yesu alivyopenda! Yesu "alisafisha" upendo wa kale na dhana/wazo la utii kutupatia mfano wa kile kilichodhamiriwa. Chukulia mifano miwili: 1) Mkono uliopooza uliponywa siku ya Sabato (Mathayo 12); na, 2) Mjadala wa Yesu kuhusu umuhimu wa kile kitokacho kinywani badala ya kile kiingiacho kinywani (Mathayo 15).)
    3. Rafiki, unapima vipi uhalisia wa 1 Yohana 2:9-11? Matendo yako yanasema nini kuhusu moyo wako? Je, unamchukia mtu yeyote? Una vinyongo na watu? Mtizamo wako ni upi kwa familia ya Mungu? Jibu la maswali haya linaonyesha kama upo kwenye njia yenye "nuru" au njia yenye " giza ".

 
 

  1. Wiki Ijayo: Kutembea Nuruni: Kuyakana Mambo ya Ulimwengu.