Wednesday, April 8, 2009

Uchambuzi lesoni ya 2: Imani

Somo hili la lesoni limetafsiriwa kutoka Corp. 2009, Bruce N. Cameron J. D. Aidha, somo hili pia linaweza kupatikana kutoka www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza.

Somo la 2: Imani

Waebrania 11, Zaburi 19, Yohana 20, 1 Petro 1, Luka 8

Utangulizi: Tunaambiwa ya kwamba imani siyo ushawishi wa kimantiki. Je, unakubaliana na hili? Chukulia ya kwamba wanafunzi wa Yesu waliamini Yesu angerudi wakati wa uhai wao. (Tazama 1 Wathesalonike 4:15-18). Sasa ni takriban miaka 2,000 baadaye. Nimewasubiria watu ambao wamekuwa wakichelewa, na nimekuwa nikichelewa. Kwa juu habari hiyo inaonkana kuwa kituko. Umewahi kuamini kitu chochote ambacho kamwe hakikuleta mantiki? Kitu ambacho hakina chembe ya ushahidi? Haya tunayaita kuwa ushirikina. Biblia inasema nini juu ya imani? Je, ni zaidi ya ushahidi? Je, tutarajie kusubiria maelfu ya miaka bila kuwa na uthibitisho vyovyote iwavyo kwamba sisi siyo wapumbavu? Au, imani ina mzizi wa kishuhuda ambao twaweza kuujenga hapo? Hebu tuingie kwenye Biblia ili tuweze kubaini!

I. Hakuna Ushahidi?
A. Soma Waebrania 11:1. Fungu hili linasema kuwa ni nini ambacho ni msingi wa kiushahidi wa imani yetu? (Matumaini yetu na vitu tusivyoviona.)
1. Mimi siyo mtaalam wa Kiyunani, lakini Waebrania 11:1 kwa Kiyunani yaelekea kusema juu ya imani kuwa ni “ushahidi usioonekana”. Je, hiyo yamaanisha kuwa watu ambao husema kuwa imani siyo ushawishi wenye vielelezo wako sahihi?
a. Au, ina maana kuwa kwa hakika kuna ushahidi wa imani, ni vile tu sisi siyo “mashahidi” kwa imani hiyo?

B. Soma Waebrania 11:3. Je, tu mashahidi katika hili? (Hapana).
1. Je, kuna kitu ambacho chaweza kuonekana hapa? (Ndiyo. Tunaona ulimwengu.)
2. Je, ni kweli kuwa ushahidi haupo katika imani yetu ya kwamba Mungu alifanya ulimwengu kwa amri yake? (Hatukuona Mungu akitenda hilo. “Amri” iliyotamkwa kwa maneno isingeweza kuonekana hata kama tungekuwa tunaangalia tendo hilo.)

C. Soma Zaburi 19:1-3. Je, Daudi na mwandishi wa Waebrania wana mtizamo tofauti?
1. Waebrania 11:3 inatuambia ya kwamba ni kwa imani pekee tunaamini kuwa Mungu aliumba ulimwengu. Mfalme Daudi anasema kuwa mbingu zinatoa kauli za uthibitisho (“zauhubiri,” “laitangaza”) juu ya Mungu wetu Muumbaji. Kila mmoja husikia na anaweza kuelewa ujumbe huu. Upi kati ya ujumbe wa Daudi na wa Waebrania una hoja nzuri zaidi?

D. Angalia mazingira yanayokuzunguka. Ushahidi unaouona kila siku unakuambia nini juu ya kama ulimwengu uliibuka au kama ulikuwa na Mbunifu Mahiri?
1. Je, ni kwa jinsi gani bustani yako inastawi bila juhudi za kibinadamu?
2. Je, ni kwa jinsi gani nyumba yako inastawi bila juhudi za kibinadamu?
3. Je, gari lako linadumu vipi bila juhudi za kibinadamu?
4. Je, kazi yako inafanikiwa vipi bila juhudi za kibinadamu? (Sijui kuhusu wewe, lakini eneo langu, nyumba yangu, gari langu na kazi yangu mara zote huhitaji uangalizi wangu-hii ni kusema kuwa haziwezi kuendelea bila “uwezo wa akili ya nje”. Kama hakuna mwanadamu ambaye angeingilia kati, vingekoma bila kutoa matokeo.

E. Mtizamo wangu ni kwamba maelezo ya kisayansi yanayoendelea sasa kuhusu ulimwengu ni The Big Bang Theory ambapo ulimwengu ulilipuka kutoka sehemu moja katika tukio moja la mlipuko. Ni nini ushahidi wa kisayansi katika hili? (Ulimwengu unatanuka sawia katika pande zake zote).
1. Je, huu pia ni ushahidi kuwa Mungu Muumbaji wakati fulani alizungumza na ulimwengu ukatokea?
2. Wanasayansi wanaamini kuwa kiwango cha utanukaji wa ulimwengu ni wa msingi Kama ungetanuka kwa haraka sana nguvu za uvutano zingefifia na ulimwengu unge “lipuka”. Na kama ungetanuka kwa pole pole sana, nguvu za uvutano zingezidi za utanukaji na ulimwengu ungesinyaa. Je, huu ni usahidi wa tukio la bahati “bang” au ushahidi wa Mbunifu ambaye kwa hakika aliweka kiwango cha utanukaji?

F. Soma Waebrania 11:4. Je, Habili hakuwa na ushahidi wa imani yake kwa Mungu? (Alikuwa na ushahidi wote uliomzunguka. Kielelezo ni kwamba Mungu aliongea moja kwa moja na Kaini na Habili (Mwanzo 4:6)).

1. Kwa hiyo, ni nini kwa hakika kilikuwa kiini cha imani ya Habili? (Imani yake ilikuwa kwa Mungu. Imani kwa Mungu ndio kilikuwa kiini cha imani ya Habili.)
2. Tunaambiwa ya kwamba Habili angali akinena. Anasema nini kwako? Kutokana na hicho anachokisema, unajenga imani yako juu ya nini? (Kisa kifupi cha Habili (Mwanzo 4:1-10) kina kila aina ya kauli kuhusu imani. Kinatuambia ya kwamba kumkataa Mungu hutuelekeza kwenye dhambi mbaya zaidi. Pia kinatuambia kwamba kumtii Mungu yaweza isimaanishe kuwa tutakuwa na maisha manyoofu. Kinapendekeza kuwa Mungu atatushindia kadri muda uendavyo).

II. Mfano wa Kwanza wa Imani: Tomaso

A. Soma Yohana 20:19-25. Je, Tomaso alikuwa na ushahidi wowote kwamba Yesu alikuwa amefufuka? (Ndiyo. Alikuwa na ushuhuda wa kuaminika wa watu kadhaa walioshuhudia).
1. Ni aina gani ya ushahidi ambao Tomaso alikuwa akiudai (Ushahidi wa kushuhudia binafsi).

B. Soma Yohana 20:26-29. Ni aina gani ya imani ambayo Yesu anaipendekeza? (wale ambao hawajaona lakini wakaamini).

1. Je, Yesu anahitaji imani isiyokuwa na tafakari wala mantiki? (Vitu viwili. Kwanza, Yesu anampatia Tomaso kwa hakika aina ya uthibitisho alioutaka. Pili, watu “waliobarikiwa” ni wale wanaoamini kwa misingi ya ushuhuda wa wengine. Yesu hahitaji wafuasi wake kuhisi kwamba alifufuka.

III. Mfano wa Pili wa Imani: Wewe

A. Soma 1 Petro 1:3-5. Fungu la 5 linatuelekeza kwetu sisi kukingwa ngao ya “imani”. Tunakingwa dhidi ya nini? (Soma 1 Petro 1:6. Imani yetu inatukinga na ukatishwaji tamaa pale ambapo maswahibu mazito yanapotokea).

1. Angalia tena 1 Petro 1:3-5. Msingi wa imani yetu ni nini? (Ya kwamba Mungu atatupatia maisha mapya katika nchi mpya. Tumaini letu katika hili limejengwa kwenye ufufuo wa Yesu kutoka katika wafu).

B. Soma 1 Petro 1:8. Je, tu mashuhuda wa ufufuo wa Yesu? (Hapana).

C. Soma 1 Petro 1:10-12. Je, hatuna ushahidi wa ufufuo wa Yesu? (Hapana. Tuna kauli ya Petro juu ya hili. Lakini, zaidi ya hilo, tuna unabii uliotimia kumhusu Yesu. Manabii wa Agano la Kale waliongea nasi pale walipoandika unabii kumhusu Yesu).

IV. Mfano wa Tatu wa Imani: Yairo

A. Soma Luka 8:40-42.je, Yairo alikuwa na imani? Imani yake ilikuwa juu ya nini? (Imani yake (tumaini?) ilikuwa ni kwamba Yesu angemponya bintiye mgonjwa).
1. Je, imani ya Yairo haikuwa na mantiki?

B. Soma Luka 8:43-49. Je, Yairo ana ushuhuda kwamba Yesu atamsaidia? (Alikuwa na ushahidi, lakini sasa ushahidi wote ni bayana na kwamba Yesu amemwangusha).

C. Soma Luka 8:50. Je, Yairo ana imani sasa kuwa Yesu atamsaidia?
1. Kama umesena ndiyo, ushahidi huo ni nini?

D. Soma Luka 8:51-56. Hali ya imani ya waombolezaji ilikuwaje kabla ya fungu la 54?
1. Angalia fungu la 56. Ni nini kiwango cha imani ya Yairo? (Wazazi wake wakastaajabu-ambayo inaashiria kuwa Yairo hakuwa na imani ya kwamba binti yake angefufuliwa kutoka katika wafu).

E. Je, kisa hiki cha mwisho kinatufundishaa nini kuhusu imani yetu kwa Mungu na hali ya ushahidi wa imani yetu? (Kwanza, inatuonyesha kwamba hata kama ushahidi unaonyesha kuwa Mungu ametuangusha, imani yetu sharti isubirie wakati/muda muafaka wa Mungu. Pili, Yairo alikuwa na ushahidi katika nguvu za Yesu-endapo ni kwa sababu ya uponyaji wa yule mwanamke aliyemchelewesha Yesu hadi kusababisha binti yake akafariki. Kilichotakiwa kwa imani isiyoonekana kilikuwa ni kiwango cha muujiza-ufufuo!)

F. Rafiki, kuna ushahidi mwingi wa imani. Je, waweza shikilia imani yako, hata kama hauna ushahidi ulioshuhudiwa kwa macho, au kile ukionacho ni ushahidi tofauti? Kama ukisubiria, kwa imani, Yesu atakupa uzima wa milele kama ukijihisi unaanza kutia shaka tazama ulimwengu na uumbaji na ujiulize kama vitu hivi vingeweza kuwepo kwa bahati.

V. Wiki Ijayo: Tumaini

Imefasiriwa na kutumwa na Mgune Masatu.

No comments:

Post a Comment