Sunday, April 26, 2009

Lesoni Somo la 5:- Ufunuo

(Warumi 1, Waebrania 1 & 4, Yohana 16)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kizulu, nk.

Utangulizi: Je, inaleta mantiki kwamba kitu chochote kile hata kama ni chenye mkanganyiko na kigumu kuelewa kama ulimwengu, au hata yenye mkanganyiko na ngumu kuelewa kama jinsi ulivyo, ya kwamba vilitokea kwa bahati? Je, haileti mantiki zaidi kuamini kwamba magari ya kifahari yanayojulikana kama “Jaguars” yanaungwa/yanatengenezwa na sokwe (ambao ni wanyama), basi kuamini kuwa ulimwengu ulitokea kwa bahati? Maswali yenye mantiki zaidi ni haya: Ni Mungu wa aina gani tuliye naye? Je, ameamua kuzungumza na wanadamu na kuwaelezea kumhusu yeye mwenyewe? Je, twawezaje kupata ujumbe wake? Hebu tuingie kwenye kujifunza Biblia na kuona kile inachofunua juu ya haya maswali yote!


I. Baadhi ya Vitu vi Dhahiri!

A. Soma Warumi 1:18-19. Popote pale fungu linapoanza na “ghadhabu ya Mungu” huwa hujikuta ninakwepa! Kwa uhakika, Mungu anasikitishwa juu ya nini hapa? (Mungu anawakasirikia wale wanaouficha ukweli wake. Paulo aweza kuwa anasema mojawapo ya vitu viwili: 1) Waovu wanamkana Mungu kwa sababu matendo yao maovu yana kawaida ya kuuficha ukweli juu ya Mungu; au, 2) Wale wanaoukana uwepo wa Mungu hufanya hivyo kwa sababu ni waovu).

B. Soma Warumi 1:20. Kwa hakika ni kwa nini waovu hawako sahihi juu ya Mungu? (Uwepo wa Mungu ni wa dhahiri kutokana na kile alichokiumba).

1. Je, unakubali ya kwamba uumbaji humfunua Mungu? (Sabato iliyopita niliona sinema nzuri ajabu juu ya suala hili. Msemaji ni Louis Giglio na sinema hiyo inaitwa “Jinsi Mungu Wetu Alivyo Mkuu.” Unaweza kutizama sehemu ya kwanza ya sehemu kadhaa kwenye tovuti ya YouTube: http://www.youtube.com/watch?v=_82lZ2PpYQE&feature=related

2. Tambua Paulo anasema pia kuwa “hata wasiwe na udhuru”. Udhuru wa nini? Kumwamini Mungu, au kuamini kwamba Mungu ana ujumbe kwa ajili yetu? Nukuu ya Paulo kwa “asili ya kimbingu” ya Mungu inajenga hoja kuwa uasili huwasilisha baadhi ya ujumbe sahihi).

C. Soma Warumi 1:21-23. Ni ujumbe gani wa kwanza sahihi tunaoweza kujifunza kutokana na uumbaji? (Kwamba kwa kuwa kuna Mungu Muumbaji, inabidi tumtukuze na kumshukuru kwa uumbaji. Kutokana na hilo basi katika tafakari ya kawaida kinachofuata ni kwamba tusiabudu sanamu ya kitu kilichoumbwa, bali tumwabudu Muumbaji mwenyewe).

D. Hebu turuke mafungu kadhaa kwenye ujengaji hoja wa Paulo kuona ni jinsi gani zaidi anatumia wazo hili. Soma Warumi 1:26-27. Paulo anamaanisha nini anaposema “mahusiano ya asili?” (Kile kinachomaanishwa na asili ya vile tulivyoumbwa).

1. Ni jinsi gani uumbaji unatufundisha kuwa ushoga ni kosa? (Nilisikiliza ombi la fedha lenye hisia kali kwa ajili ya kurekebisha mazingira ili kwamba wale dubu wanaopatikana kwenye maeneo ya barafu wasiweze kupotea duniani. Naweza kubashiri, kwa akili ya kawaida, kwamba mojawapo ya masuala ya “kimazingira” ni kuwaambia hao dubu wasijihusishe na ushoga. Kwa hakika, wale waliokuwa wakiomba fedha hawakuwa na kitu kama hicho akilini. Lakini, naamini unaelewa dhana ya Paulo ya “mahusiano ya asili”.


II. Wasemaji!

A. Soma Waebrania 1:1. Fungu hili lasema kuwa Mungu anawasilianaje na wanadamu?

1. Hebu tizama mbadilishano huu. Paulo anatuambia tuangalie na kupata ujumbe kutoka kwa Mungu. Waebrania inatuambia kuwa Mungu aliongea nasi kupitia kwa manabii. Hoja ya uumbaji ni dhahiri. Ni sababu gani iliyo “dhahiri” tuliyonayo kuamini kuwa manabii walikuwa wakiongea kwa niaba ya Mungu? (Vitu viwili. Kwanza, kama uumbaji ni uthibitisho wa Muumba, je, siyo mantiki kwamba Muumba angetaka kuongea nasi? Pili, ujumbe wa manabii una mwelekeo ule ule. Kundi la watu wenye kujikweza nafsi katika karne kadhaa kwa uongo walidai kuongea kwa niaba ya Mungu, ungewatarajia kuwa na ujumbe mwingi kwa kadri ambavyo wajumbe wangekuwepo. Ujumbe wa moja kwa moja na usiobadilika unapendekeza kuwa umetoka kwenye chanzo kimoja).

B. Soma Waebrania 1:2-3. Kwa nini tuamini ya kwamba Yesu ni Mungu? (Kwanza, Yesu alidai kuwa ni Mungu (Mathayo 26:63-64; Yohana 12:44-46). Pili, ufufuo wake ulikuwa si kama kitu chochote kile kilicho ndani ya uwezo au mamlaka. Hili kwa hakika ni suala la “Mungu”.

1. Ni ujumbe gani kutoka kwa Mungu tulioupokea kupitia kwa Yesu? (Yesu anasema kuwa kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba yangu. Yohana 8:19. Kama tukijifunza maisha ya Yesu, tunaelewa asili ya Mungu.


III. Hebu Litazame!

A. Soma Waebrania 4:12-13. Wangapi kati yenu mnaweza kuelezea Biblia katika nyumba zenu kama “kitu kilicho hai na chenye nguvu” kinyume na “wazoa taka?”

1. Hebu tazama lugha iliyotumika “tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo”. Mada yetu inahusu kama kweli Mungu hujifunua kwetu. Ni jukumu gani linapendekezwa kuwa linafanywa na Biblia katika ufunuo huu? (Sisi sote tuna mawazo na makusudio ya moyo [mitizamo] ya jinsi gani inatupasa kuishi na kuwajali wengine. Biblia hujaribisha/huthibitisha mawazo haya na mitizamo hii dhidi ya viwango vya mwenendo wa Mungu).

2. Umewahi kusema kuwa “Natamani kwamba Mungu angefunua mapenzi yake kwangu” kwa chochote kile ukitamanicho kwa wakati huo?

a. Kama jibu lako ni “Ndiyo” je, umetizama kile Mungu alichokisema kuhusu mada hii kutoka kwenye maandiko ya Biblia? Kama jibu ni hapana, je, ulihitaji kweli kujua/kufahamu mapenzi ya Mungu?

B. Soma 2 Timotheo 3:16-17. Chanzo cha Biblia ni nini? (Mungu).

1. Biblia inaweza kuchukua jukumu gani katika kufunua mapenzi ya Mungu maishani mwetu? (Maneno “mafundisho, maonyo, kuongoza na kuadibisha” yanaonekana kujumuisha nyanja zote za maisha).


IV. Sikiliza!

A. Soma Yohana 16:7-9. “Msaidizi” ni nani? (Roho Mtakatifu).

1. Je, Richard Dawkins (mtu asiyemwamini Mungu) naye anasumbuliwa kidhamira kuhusu dhambi zake? (Tambua ya kwamba fungu la 9 linasema kuwa Roho Mtakatifu huwafanya kujisikia hatia hata wale wasioamini uwepo wa dhambi! (Au angalao basi hata wale wasiomwamini Yesu)).

B. Soma Yohana 16:10-11. Je, umewahi kujisikia hatia kwa dhambi hapo siku za nyuma? Umewahi kujisikia hatia siku za nyuma juu ya kile unachopaswa kukifanya kuhusu dhambi zako?

1. Kama umejibu “Ndiyo” kwa lolote kati ya hayo maswali mawili, je, huo ni uthibitisho wa ziada kuwa Mungu yupo na kwamba anajihusisha kwa dhati kabisa katika kuwasiliana na wanadamu?

2. Hili ni tatizo jingine linalowasumbua wale wanaoamini kuwa mwanadamu hakuumbwa bali alitokana na mabadiliko/mageuko ya pole pole kuanzia kwa mnyama. Kwa nini tukuze dhamira? Kwa nini hili “lundo la nyama” linaloendesha kazi za mwili liwe na mawazo yoyote zaidi ya kile ambacho ni muhimu kwa ajili ya kustahimilisha maisha?

a. Chanzo cha dhamira ni nini? Kama hatukuikuza, basi ni lazima iakisi nguvu zilizo nje ya uwezo wa mwanadamu, sawa?

C. Soma 1 Timotheo 4:1-4. Je, twaweza kuwa na dhamira mbaya? Dhamira inayotuambia kuwa tusifanye vitu ambavyo vinakubalika kwa usahihi kabisa kufanya?

a. Je, wawezaje kutenganisha kati ya mawazo yako mwenyewe na ya Roho Mtakatifu anayenena nawe?

b. Je, wawezaje kutenganisha kati ya “roho wadanganyao na mambo yanayofundishwa na mapepo” na Roho Mtakatifu anayenena nawe?

D. Soma Mathayo 12:31-32. Kukufuru dhidi ya Roho Mtakatifu inamaanisha nini? Je, ina chochote cha kuhusianisha na kukanganya ujumbe wa Roho Mtakatifu na jinsi unavyofikiri wewe binafsi au inakanganya na majaribu ya kimapepo? (Ili kusaidia kubaini hili, tunahitaji kuangalia kuanzia kwenye msingi).

E. Soma Mathayo 12:22-24. Yesu alikuwa anaonyesha nini pale aliporejea juu ya kuongea dhidi ya Roho Mtakatifu? (Yesu anawaonya wale wanaohusianisha kazi ya Roho Mtakatifu na kazi ya Shetani.

1. Kwa nini hii iwe dhambi isiyosamehewa? Kwa nini kusema mambo mabaya kwa upande mmoja wa Utatu Mtakatifu iwe mbaya zaidi kuliko kusema mambo mabaya juu ya upande mwingine wa Utatu Mtakatifu?

F. Soma 1 Samweli 3:12-14. Mungu anatoa ujumbe kupitia kwa Samweli kwa Kuhani Mkuu Eli kuhusu wana wake wa kiume, makuhani. Je, huu pia ni mfano mwingine wa dhambi isiyosamahewa? Kama ni hivyo, je, kuna dhambi ngapi zisizosameheka zilizopo? (Sidhani kama kuna dhambi iliyopo isiyosameheke kivile. Kumbuka ya kwamba wana wa Eli walikuwa na jukumu pamoja na kushughulikia hatua za kufuatwa kwa ajili ya msamaha wa dhambi pale hekaluni. Walikuwa wameshikilia mzani wa mchakato wa msamaha wa dhambi. Kwa kuwa walitumia vibaya mchakato huo, wasingeweza kusamehewa. Mtizamo huo huo ndio uliopo wa “kumsononesha” Roho Mtakatifu. Ni sehemu ya muhimu sana katika mchakato mzima wa msamaha wa dhambi-hututia nafsi zetu hatiani kuhusu dhambi zetu.

G. Soma Tito 1:15-16. Unapoharibu dhamira yako, je, wajipenyeza sehemu ambayo, kivitendo, dhambi yako haiwezi kusamehewa kwa sababu umeharibu mchakato mzima?

H. Baada ya kuwa tumesema kwamba tunaweza kuharibu kazi ya Roho Mtakatifu, hebu turejelee kwenye suala letu ambalo hatukufikia muafaka wa jinsi gani tunaweza kutofautisha kati ya ujumbe wa Roho Mtakatifu unaotujia kupitia kwenye dhamira zetu na ujumbe mwingineo. (Soma tena Yohana 16:15. Roho Mtakatifu huchukua ujumbe wake kutoka kwa Mungu. Kwa hiyo, Ujumbe wa Roho Mtakatifu ni lazima uwe sawa na ujumbe mwingineo unaofunuliwa kutoka kwa Mungu-kupitia kwenye maandiko ya Biblia, manabii wa kweli na asili).

I. Kiwango chako cha tahadhari kwenye ujumbe wa Roho Mtakatifu kipo vipi? Unaweza kusikia sawia? Au ujumbe huwa umekuwa barely discernable?

J. Rafiki, tunaye Mungu anayehitaji kuwasilisha mapenzi yake kwetu. Je, utaambatana na ujumbe wake na kuhuisha maisha yako kufuatana na ujumbe huo? Je, utamsikiliza Roho Mtakatifu na kuwa tayari na muwazi kwa mwongozo wake?


V. Wiki Ijayo: Dhambi.

Somo hili limefasiriwa na kuandaliwa na
Mgune Masatu.

No comments:

Post a Comment