Thursday, April 16, 2009

Lesoni Somo la 3: Tumaini

(Zaburi 33, 39, 43, 71 & 146, 1 Petro 1)

Somo hili la lesoni limetafsiriwa kutoka Corp. 2009, Bruce N. Cameron J. D. Aidha, somo hili pia linaweza kupatikana kutoka www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza.

Utangulizi: Je unahisi matumaini yako yanapotea? Nilipokuwa katika umri wa miaka 20 na kitu niliamini kwamba Marekani ilikuwa ikielekea kwenye machweo. Kwa nini isiwe hivyo? Mataifa yote huinuka na kuanguka, kwa nini sisi isiwe hivyo? Kisha, Ronald. Reagan alichaguliwa rais na mtazamo wangu ulibadilishwa kabisa. Nikapata matumaini katika siku zijazo za Marekani. Sasa Marekani na dunia kwa ujumla yaonekana ya kwamba vinaingia (inaingia) katika nyakati ngumu. Je ni kwa jinsi gani mkristo atazame mambo haya? Wote twaishi katika nchi tofauti, je tumaini letu la siku zijazo linategemea matumaini ya mataifa yetu.
Hebu uwe mkweli na nafsi yako, je ungependa ukae katika giza, nyumba ya upweke, ukishikilia tumaini la kiroho tu? Hebu na tutazame katika mwanga wa Biblia na kuona aina gani ya tumaini Mungu huwapa wafuasi wake!


I. Tumaini au msaada?

A. Zaburi 146:5. endapo nikikupatia tumaini au msaada ni kipi utachagua?

1. Je hivyo viwili ni tofauti?

2. Ni kwa jinsi gani fungu hili linaonyesha kwamba viwili vyote hivi hufanya kazi pamoja? (Tumaini hilo katika Mungu hutupa msaada halisi.)

B. Soma Zaburi 146:6. kwa nini mtunga Zaburi anataja sifa za Mungu mara baada ya kuzungumzia wale ambao tumaini na msaada wao ni katika Mungu? (Hii huthibitsha kuwa Mungu anaweza kutenda. Kama Mungu anaweza kuumba mbingu na nchi, anaweza kutatua matatizo yako madogo!)

C. Soma Zaburi 146:7. tazama sentensi ya kwanza. Ni kwa jinsi gani sehemu ya kwanza ya fungu hili ni tofauti na sehemu ya mwisho wa fungu hilo? (Mungu anatoa haki na anatoa chakula!)


1. Ni kwa jinsi gani Mungu analifanya hilo? (Hili huenda likahusisha msaada wako)
2. Baada ya kunithibitishia haki, na sasa natambua ya kuwa Mungu anawaachia wafungwa! Je, haki hiyo ikoje? (Kiashirio ni kwamba walifungwa kimakosa. Mungu hutoa haki halisi katikati ya uonevu wa mwanadamu.)

D. Soma 146:8. Je wafikiri tunazungumzia wale ambao ni vipofu haswa? (Twafahamu ya kwamba Yesu alimponya kipofu (Mathayo 9:27-30), lakini uzungumziaji wa wale “walioinama” hunifanya niamini ya kuwa fungu hili linazungumzia pia wale ambao mizigo yao ni mizito. Hawa ni wale ambao wamekatishwa tamaa na mazingira kiasi kwamba hawawezi kuona tumaini lolote mbele yao).

1. Je, inamaanisha nini “kuona” masuala yajayo?

2. Je, ni kwa nini fungu linaongezea kuwa, jambo lenye kuonekana kama kutohusiana, kiashirio kwamba Mungu huwapenda wenye haki? (Mungu ana mvuto kwa wale wanaomheshimu. Utiifu husaidia ufahamu mzuri wa siku zijazo).

E. Soma Zaburi 146:9. Je, wajane, wasio washiriki na yatima wana kitu gani kwa ujumla? (Ni wale walio wanyonge katika jamii. Mungu ana mvuto kwa wanyonge na huingilia kati kuwasaidia dhidi ya waovu).


F. Je, ni tumaini la aina gani ambalo tunalipata kwenye haya mafungu kutoka Zaburi 146? (Tumaini la msaada wa dhati! Mungu anaweza kusaidia. Anasaidia kwa haki na kwa chakula. Anasaidia wenye msongo. Anawasaidia wale wasio na “nguvu” katika dunia hii. Anawatafuta wale wanaomtii).


II. Tumaini Makini

A. Soma Zaburi 33:18-19. Serikali huonekana kuweka vinyaka uso (kamera) nyingi ili kuweza kuchukua matukio ya wananchi wake. Je, unapendelea/unafurahia pale Serikali inapoweka “jicho lake” kwako? Na je, ni vipi kuhusu Mungu anapoweka jicho lake kwako?

1. Tulikuwa na marafiki waliokuwa na wana wa kiume watatu. Baba alikuwa nadhifu, lakini alikuwa mtu mwenye kuwa mbali kifikra. Mkewe anakumbuka jinsi jinsi alivyomuacha mumewe kwenye sehemu ya maduka makubwa “kumwangalia” mtoto wao mdogo kwenye kiti cha kusukuma. “Baba” akavutiwa na kitu kingine na hivyo akamwacha mtoto peke yake pale kwenye duka kubwa. Pale “mama” aliporudi na kumkuta mtoto peke yake pale madukani-kwa hakika kilikuwa kituko kilichosimuliwa mara nyingi! Je, ni nini kinachokujia/unachofikiria pale Mungu anapokuhakikishia kwamba anakuangalia? (Habari njema ni kwamba Mungu anafahamu kile ninachopitia. Anakuwepo pale ninapokumbana na matatizo na ananipenda).

B. Soma Zaburi 33:20-21. Kwa nini fungu linatumia neno “ngojea?” (Inaonyesha kwamba si mara zote Mungu anatekeleza ratiba zetu).

C. Soma Zaburi 33:22. Kwa nini unafikiri mtunga Zaburi anaelezea upendo wa Mungu kama “usioshindwa” katika muktadha huu? (Mungu ni msaada wetu na ngao yetu. Mara nyingine, yaweza kuonekana kuwa msaada na ngao havipo-hivyo kuwa sababu ya kungojea kwetu na tumaini letu. Mwandishi wa Zaburi anatuambia ya kwamba upendo wa Mungu haushindwi kutuhakikishia ya kwamba msaada unakuja).


III. Tumaini kwa Tabia Zetu

A. Soma Zaburi 39:7-8. nilipokuwa mdogo walimu wangu walinifundisha ya kwamba Mungu angenisamehe dhambi zangu, lakini ingenipasa kutaabikia matokeo ya dhambi. Ni tumaini la aina gani linaloongelewa katika mafungu haya?(Tunaweza kutumaini tu ya kwamba kiwango chetu kamili cha dhambi zetu hakitotufedhehesha. Mungu kwa ukarimu wake mara nyingine ametukinga dhidi ya matokeo kamili, yenye kufedhehesha ya dhambi zetu.)


B. Soma Zaburi 39:10-11. Je Mungu hutuepushia matokeo ya dhambi zetu? (Mungu huweza kutukinga dhidi ya kejeli za wadhambi wenzetu ikiwa ni matokeo ya dhambi zetu, lakini Mungu hutuadabisha kwa manufaa yetu wenyewe.)

IV. Tumaini katika hali yenye kukatisha tamaa

A. Soma Zaburi 43:5. Je waelewa ni nini mtunga Zaburi anasema? Je, umewahi kupitia nyakati ambapo moyo wako umenyong’onyea na unahisi na kukosa furaha na mwenye kusumbuliwa?
B. Ni nini tumaini letu katika nyakati hizo? (Ya kwamba Mungu atatuokoa katika kukata kwetu tama na huzuni zetu. Pengine huenda kumsifu Bwana ni mojawapo ya mwanzo wa suluhisho. Binafsi kumsifu Mungu huhuisha nafsi yangu.)


V. Tumaini katika umri mkubwa

A. Soma Zaburi 71:9. Je ni kwa jinsi gain tumaini hubadilika kwa kadiri uzee unapokuja?

1. Fikiria kwamba ungekuwa unategemea wengine kwa mahitaji yako mengi katika maisha yako. Ni kwa jinsi gani hiyo ingeathiri mtazamo wako?

B. Soma Zaburi 71:10-12. Inaonekana kwamba mfalme Daudi ndiyo mwandishi wa hili (komentari zinatofautiana katiaka jambo hili), na anahofu na maadui zake wa kisiasa. Je, inaweza kuwa hii ni hofu tu ya mfalme mzee, au inawezekana jambo hili linaweza kutokea hata kwa wafanyakazi wazee?
1. Je inawezekana jambo hili huambatana na umri mkubwa?
2. Je bado tuna tumaini hata katika umri mkubwa? Na ni nini ni tumaini letu? (tumaini letu lippo katika Bwana, na nia yake ya kutuokoa mapema.)


VI. Tumaini katika wokovu

A. Mpaka sasa tumekuwa tukijifunza nini Biblia kuhusu tumaini katika Bwana kwa msaada wa hakika na thabiti katika maisha yetu.

B. Soma Tito 1:1-3. ni nini tumaini la maisha yetu katika muktadha wa maisha yetu ya kikristo. (Ya kwamba tutapata uzima wa milele.)
1. Ni katika nini tumaini letu la maisha ya milele hujengwa? (Kabla ya mwanzo wa wakati Mungu aliweka ahadi kuwapa wanadamu maisha ya milele. Yesu alifaulu katika ahadi hiyo.)

C. Soma Petro 1:3-5. Mbali na uzima wa milele, ni tumaini gani lingine tulilo nalo kuhusu mbingu? (Ya kwamba kutakuwa na urithi usioharibika.)
1. Na kwa wakati uliopo nini kinaendelea kwetu? (1 Petro 1:5 hutuambia kwamba kupitia amani tunalindwa na nguvu za Mungu mpaka wokovu wetu ufike! Pamoja na matatizo tuliyonayo tuna tumaini la uzima wa milele.)


VII. Utukufu na tumaini

A. Tu wenye baraka kiasi gani! Tunaweza tukawa na tumaini katika Bwana kwa msaada kwa sasa na pia tuna tumaini kwa uzima wa milele wa utukufu. Hii yote huwezekana kupitia Yesu. Tufanye nini kwa sasa? (Soma 1 Yohana 3:2-3. tunajitakasa.)
1. Humaanisha nini sisi kujitakasa? Ni Mungu tu ndiye mtakatifu. (Tunapaswa kujibidisha, kwa uweza wa roho mtakatifu, kwa fikra sahihi na maisha sahihi.)

B. Rafiki habari gani kwako? Je unapitia matatizo katika maisha yako? Mungu anakupatia matumaini na msaada hapa duniani na sasa – katika ratiba yake, na si yako. Muhimu zaidi, Mungu hutupa tumaini kwa maisha ya milele. Je, unaishi kama mtu mwenye matumaini kwa Mungu?


VIII. Wiki ijayo: Uzima.


Somo hili limetafsiriwa na kuandaliwa na
Masatu Mgune

No comments:

Post a Comment